Page 122 - EDK_F5
P. 122

SURA YA TATU                                                            NGUZO ZA IMANI

        Kwa kuweka bayana suala kama hili aliulizwa Mtume Muhammad (S.A.W) kwa kuwa
        Allah  (S.W)  kishakadiria  kila  kitu  ipo  haja  ya  kufanya  amali? Akajibu  katika  Hadith
        ifuatayo:

                Kutoka  kwa  Ali  (R.A),  amesema: “Siku  moja  Mtume  wa  Mwenyezi
                Mungu (S.A.W) alikuwa amekaa, na mkononi mwake alikuwa na fimbo
        FOR ONLINE READING ONLY
                akaigonga  ardhini  kwa  nguvu,  akainua  kichwa  chake  na  kusema:

                Hakuna nafsi yoyote kati yenu isipokuwa inajulikana mahala pake baina
                ya Pepo na Moto, wakasema: Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu, kwa
                nini sasa tunafanya Amali? Hivi hatukai tu (tukaacha amali)? Akasema:
                Hapana, fanyeni,  kwani  kila  mtu amerahisishiwa yale  aliyoumbiwa
                kwayo, kisha akasema: Yule anayetoa (zaka, sadaka na vingenevyo)

                na kumcha Mwenyezi Mungu. Na kusadiki jambo jema (akalifuata).
                Tutamsahilishia njia ya kwenda Peponi. Na afanyiaye ubakhili, viumbe
                wenzake. Na akakadhibisha (asiyafanye)  asiwe na haja ya mambo

                mema. Tutamsahilishia njia ya kwendea Motoni. (Bukhari na Muslim).

        Kwa hiyo, mja  atakapofanya  maasi  kama  kuacha kuswali, kuzini,  kunywa ulevi  na
        mengineyo basi ataandikiwa dhambi na kuadhibiwa kwa kuwa kayafanya kwa hiari yake

        bila ya kulazimishwa.

        Pili, Kutoamini Qadari inapelekea kutokamilika imani ya mja na kuwa kafiri, kama
        ilivyokuja katika Hadith ya Mtume Muhammad (S.A.W):

                Kutoka kwa Jabir bin Abdullah amesema: Mtume wa Mwenyezi Mungu
                (S.A.W) amesema: “Hakuna mja mwenye imani mpaka aamini Qadari za
                kheri na shari zake, mpaka ajue kwamba lililompata halikuwa limkose,
                na lile alilolikosa halikuwa alipate”. (Tirmidhy na Ahmad).






















                                                 112
   117   118   119   120   121   122   123   124   125   126   127