Page 123 - EDK_F5
P. 123

SURA YA TATU                                                            NGUZO ZA IMANI

         Zoezi la 3 1

          Jibu maswali yafuatayo kwa ufupi

          1. Soma aya ifuatayo kisha  eleza aya hiyo inahusu jambo gani

        FOR ONLINE READING ONLY
                                                                          َ
                                                   ۡ ۡ
                                                                    َ
                                           َ َ
                                                                           ٓ
                              َ
                   ۡ َ
                                                                               َ َ
                                  َّ
                                        ۡ ۡ
                                                             َ ُّ َ َ
                                                                        َ ۡ
                                     َ َ
                                         َ
                        َ َ ً
                  َ ُ َ
                                                                            َّ
                                                         َ
                                               َ َ
                                                                   ۡ
                              ٰ
                                                                                 ٰ
                 ٰ
                                                                      ٰٓ
                 قلتف رخاء اهلِإ ِللٱ عم لعت لو ِۗةمكِلٱ نِم كبر كلِإ حوأ امِم كِلذ
                                                               ً ُ ۡ َّ ٗ  ُ  َ َ َّ َ َ
                                                            ٣٩اروحدم امولم منهج  ِ ف
                 Haya ni katika yale aliyokufunulia Mola wako katika hikima (zake).
                 Wala usimueke pamoja na Mwenyezi Mungu, mungu mwengine, usije
                 kutupwa katika Jahanamu hali ya kuwa mwenye kulaumiwa (na)
                 mwenye kufukuzwa (huku na huku). (Israa, 17:39)
         2.  Eleza dhana ya uungu kwa mujibu wa mafundisho ya  Qur’an
         3.  Fafanua maana ya kuamini Qadar ya Allah (S.W)
         4.  Onesha namna mtazamo potofu juu ya Qadar unavyoathiri  jamii yako
         Ufupisho
         Allah (S.W) ameumba ulimwengu na vilivyomo ikiwa ni dalili ya kuwepo kwake na
         Yeye ndiye anayestahiki kuabudiwa. Imani ya mja haikamiliki mpaka aamini nguzo
         sita za imani ambazo zinategemeana, na kama mtu atakanusha moja katika hizo basi
         mtu huyo atakuwa kafiri na ataadhibiwa siku ya Kiyama.
         Mja anapoamini nguzo sita za imani hupata athari kubwa katika utekelezaji wa amali
         zake,  na humpelekea  kwenye uchamungu  na hatimaye  kupata  malipo  mema  kwa
         kuingizwa peponi.

         Ama kwa wale wenye matazamo potofu wa kuamini nguzo hizo basi unawapelekea
         kukanusha nguzo hizo na kuwa ni miongoni mwa watu waliopotea na kupata  hasara
         kubwa, na malipo yao ni motoni.


















                                                 113
   118   119   120   121   122   123   124   125   126   127   128