Page 202 - EDK_F5
P. 202

SURA YA SABA                                          UTEKELEZAJI WA NGUZO ZA UISLAMU

        (R.A), aliwapiga vita watu wa Yamama kwa kukataa kutoa zaka, kwani alisema hakuna
        kutofautisha baina ya nguzo ya swala na nguzo ya zaka.

        Katika  utekelezaji  wa nguzo ya Hijja,  pia hutekelezwa  nguzo nne zilizobakia,

        Mahujaji,  wawapo katika  viunga  vya  Makka,  wakitekeleza  nguzo  ya  Hijja,  takribani
        FOR ONLINE READING ONLY
        huwa wanatekeleza pia nguzo zote za Uislamu. Yaani, wanatamka shahada kwa kukariri
        mara kwa mara, wanaswali, wanatoa zaka na wanafunga hasa kwa mtu aliyevunja miiko
        ya hijja, anapaswa afunge siku 10, tatu akiwa hijja na saba akirejea nyumbani kwao.
        Hii ni ishara kwamba nguzo za Uislamu zina uhusiano mkubwa katika utekelezaji wake.
        Hujaji  anapofunga  safari  kwa ajili  ya  Hija,  huwa tayari  kutengana  na  familia  yake,
        ndugu, jamaa na rafiki zake kwa kipindi chote cha safari na huwa tayari kukabiliana na
        misukosuko na magumu yote ya safari na huwa tayari kufuata barabara masharti ya Ihram
        na masharti yote ya hijja kwa ujumla kwa ajili tu ya kutafuta radhi za Allah (S.W). Pia,
        Hija inamzoesha Muislamu kuwa tayari kujitoa muhanga kwa mali yake na nafsi yake
        kwa ajili ya kusimamisha dini ya Allah (S.W). Kwa mawanda ya kijiografia nguzo hii ndio
        nguzo kubwa kwa maana hubeba uhalisia wa mahusiano ya Waislamu kimataifa, wakiwa
        na sare moja (Ihram), lugha moja, hotuba moja (Arafa) , na matendo yote hufanyika kwa
        hali ya usawa bila matabaka ya rangi, kabila wala taifa.

        Utekelezaji  wa nguzo zote hujenga uhusiano wa karibu wa mja na Allah (S W)
        pamoja na viumbe vyake, mwanadamu anapaswa kujenga uhusiano mzuri baina yake
        na Mola wake Mlezi na baina yake na viumbe vya Mola wake. Uhusiano wote wa aina
        mbili hujengeka kwa kutekeleza nguzo za Uislamu. Kwanza, shahada inamuunganisha
        mja na Mola wake kwa kukataa kumuabudu yeyote kati ya viumbe vyake ila Yeye tu. Pili,
        swala humkataza mja na maovu na machafu, kwa kukatazika huko atakuwa na uhusiano
        mzuri na Mola wake Mlezi pamoja na jamii inayomzunguka kwa kuwa na tabia njema.
        Tatu, zaka inayolenga kutakasa nafsi ya mtoaji, mali ya mtoaji na jamii ya Kiislamu,
        inajenga uhusiano mwema baina ya mtoaji na Mola wake, na mtoaji na jamii yake. Nne,
        Saumu inayomwandaa mja kuwa mchamungu pia inaleta uhusiano imara kati ya mfungaji
        na Mola wake na mfungaji na jamii yake, kwani mchamungu huwa na tabia na mwenendo
        mzuri unaoridhiwa na Mola wake Mlezi pamoja na unaokubalika na jamii yake. Tano,
        hijja inayomuandaa Hujaji kumtumikia Mola wake Mlezi, nayo ina nafasi kubwa katika
        kuibua uhusiano baina ya hujaji na Mola wake, na Hujaji na jamii yake, kwani hujaji
        hana hiari ila kutii maamrisho na kuacha makatazo ya Allah (S.W), jambo ambalo huleta
        uhusiano mwema baina yake, Mola wake na viumbe wa Allah (S.W).









                                                 192
   197   198   199   200   201   202   203   204   205   206   207