Page 204 - EDK_F5
P. 204

SURA YA SABA                                          UTEKELEZAJI WA NGUZO ZA UISLAMU

        Itikadi, katika sharti hili humtaka anayetekeleza nguzo za Uislamu itikadi yake iwe ni
        Uislamu na ndio maana katika kuzipanga nguzo za Uislamu, Shahada inachukuwa nafasi
        ya kwanza kama msingi wa utekelezaji wa nguzo nyingine. Kwa hiyo, hata kama mtu
        ataamua kuswali usiku kucha, kufunga mwaka mzima au kutoa mali zake zote ikiwa
        itikadi yake sio Uislamu basi hesabu zake zote zimepotelea patupu. Sharti hili huwagusa
        FOR ONLINE READING ONLY
        hata wale waliotamka shahada pindi wanapojiingiza katika shirki basi hubatilisha itikadi
        yao na hivyo matendo yao pia hupeperuka.

        Nia,  sharti  hili  hulenga  kusudio la  ndani  alilonalo  Muislamu  wakati  wa kupanga  na
        kutekeleza jambo, linaweza pia kuitwa dhamira, dhumuni au msukumo wa ndani. Yaani

        anafanya kwa ajili ya nini au kwa ajili ya nani na ili iweje. Kama ilivyoelezwa katika
        mada tangulizi kuwa mwanadamu aliyetia nia ya kufanya ibada na akafanya kila juhudi
        kukamilisha ibada hiyo na hakufanikiwa, basi hulipwa malipo sawa na yule aliyetekeleza
        kwa ukamilifu. Funzo linalopatikana hapa ni kwamba mwanadamu amepewa uhuru wa
        kuchagua kati ya kheri na shari, hivyo, ni juu yake kuamua. Kwa kuwa kiumbe huyu muda
        mwingine anaweza kusema asichomaanisha, au kutenda na kusifia kile anachokichukia

        moyoni basi Allah (S.W) ameepukana na udhaifu wa kuhadaiwa, hujua ya siri na dhahiri.
        Japo mbele  ya macho  ya  wanadamu  mja  huyu ataonekana  mwema  na atadhaniwa  ni
        mwenye kustahiki malipo makubwa, mbele ya Allah (S.W) ataonekana katika uhalisia
        wake. Ndio maana imeelezwa kuwa siku ya kiyama watu watakimbiana kwa kuwa kila
        mmoja yapo aliyoyafanya nafsi yake ikijua fika ni ria na hakukusudia kulipwa siku ya
        hukumu:

                Kutoka kwa Umar Ibn Al Khatwab (RA) ambaye amesema: Nilimsikia
                Mtume wa Allah akisema: Bila shaka amali inategemea nia, na kila mtu
                atapata kwa mujibu wa kile alichokinuia. Mtu ambaye hijra yake ni kwa
                ajili ya Allah (S.W)  na Mtume Wake (S.A.W), basi hijra yake ni kwa ajili
                ya Allah (S.W) na Mtume Wake (S.A.W), Na ambaye hijra yake ni kwa
                ajili ya manufaa ya kidunia au kwa ajili ya kumuoa mwanamke, basi
                hijra yake ni kwa lile aliloliendea.   (Bukhari na Muslim)

        Baadhi ya wanachuoni wamechukulia Hadith  hii kuwa ni  theluthi ya Uislamu; kwamba
        muumini hulipwa kutokana na nia yake na uzuri wa amali yake, mwenye kuwa na matendo
        mazuri na ikhlasi juu ya matendo hayo, atalipwa kutokana na usafi wa nia yake na ikhlasi
        yake; na mwenye kufanya amali nzuri kwa kujionyesha kwa watu na si kwa ajili ya Allah
        (S.W) basi amali hiyo itarejeshwa hata kama ni kubwa. Kwani sharti ya kukubaliwa amali
        njema ni usafi wa amali  hiyo na iwe ni  kwa ajili ya Allah (S.W). Pia iwe imewafikiana
        na mwongozo wa Mtume Muhammad (S.A.W).


                                                 194
   199   200   201   202   203   204   205   206   207   208   209