Page 203 - EDK_F5
P. 203

SURA YA SABA                                          UTEKELEZAJI WA NGUZO ZA UISLAMU

         Zoezi la 7 1
          1.  Kwa kutumia mchoro ainisha uhusiano wa nguzo za Uislamu

          2.  Fafanua nguzo za Uislamu kwa kuzingatia lengo la kila nguzo

          3.  Shahada mbili ndio kiingilio cha Uislamu.Thibitisha
        FOR ONLINE READING ONLY
          4.  Kwa kuzingatia utekelezaji wa nguzo za Uislamu, onesha uhusiano uliopo kati ya :
             (a) Mja na Allah(S.W)

             (b) Nguzo moja na nyingine



        Uhusiano wa masharti, matendo na malengo ya nguzo za Uislamu

         Kazi ya 7 2


         Shirikiana na mwenzako chunguza uhusiano wa matendo na masharti ya Hija na nguzo
         zingine za Uislamu kisha wasilisha kwa wanafunzi wenzako darasani


        Katika utekelezaji wa nguzo za Uislamu takribani kila nguzo ina masharti na matendo
        ambayo yakitekelezwa ipasavyo kwa mjumuiko wake, ndio hupelekea kufikiwa kwa lengo
        la nguzo husika. Kwa kuwa mlengwa ni mmoja anayewajibika kutekeleza nguzo zote na
        kama ilivyofafanuliwa hapo awali kuwa mlengwa huyu analo lengo la kuumbwa kwake

        na nguzo hizi ni nyenzo tu zitakazo mfikisha katika ukamilifu wa lengo na hadhi.   Kwa
        ngazi hii ya Elimu ya dini ya Kiislamu,  kipengele hiki kinafafanuliwa kwa muhtasari wa
        kiuchambuzi kwani ngazi zilizotangulia kila nguzo ya Uislamu imechambuliwa kwa kina.


        Masharti ni jumla ya mambo ambayo inamlazimu Muislamu ayatekeleze ili ibada husika
        ikubaliwe. Katika kufafanua uhusiano wa masharti, yapo yanayojitokeza katika utekelezaji
        wa kila nguzo na yapo masharti kwa baadhi ya nguzo kama ifuatavyo:

        Utimamu wa akili, baleghe na Afya, ibada zote hufanywa kwa lengo la kuhitaji radhi

        na malipo kutoka Allah (S.W).  Hivyo katika mjumuiko wa watu wapo ambao hawana
        wajibu wowote, kutokana na kukosa sifa ya sharti la utimamu. Watu hao ni pamoja na
        mtoto mdogo hadi atakapofikia baleghe, mwenye kichaa au maradhi ya akili hadi akili
        yake itakaporejea na vilevile mtu aliyelala usingizi atahesabika mwenye udhuru juu ya
        utekelezaji  wa ibada hadi atakapotoka  usingizini. Katika Musnad Abu Hanifa kupitia

        riwaya ya Al-Hasfiki kuna Hadith isemayo:

                ... Kalamu imezuiwa kwa watu watatu; mwenye kichaa mpaka arejewe
                na akili, mtoto mdogo mpaka abaleghe na mtu aliyelala mpaka aamke.
                                                 193
   198   199   200   201   202   203   204   205   206   207   208