Page 242 - EDK_F5
P. 242

SURA YA TISA                                                   HISTORIA KATIKA UISLAMU


        Kwa maana,wengi wao si wenye kutimiza ahadi ipasavyo. Ishara ya kuasi ahadi zao ni
        kule kuelekea katika upotofu na kwenda kinyume na mafundisho ya Mitume na vitabu
        vilivyoteremshwa kwao.

        Msimamo wa wanachuoni, tukio la ahadi ya utii limekubaliwa na kuungwa mkono na
        FOR ONLINE READING ONLY
        wanachuoni wa karne tatu bora za awali katika Uislamu. Kwa maana kila karne kuna
        mwakilishi  wa kuunga mkono kuwapo kwa tukio la ahadi hii, kwa mfano, karne ya
        kwanza kulikuwa na Ibn Abbas, karne ya pili Sa’id Ibn Jubayr (aliyetawafu 95/714), na
        al-Ḥasan al-Baṣri (aliyetawafu 110/728), ikifuatiwa na karne nyingine za baadaye. Hii ni
        kwa kuwa ahadi hii ina uhusiano wa moja kwa moja na dhana ya fitra, au asili ya awali
        ya mwanadamu, ambayo imetajwa katika Qur’an (30:30). Kwa mujibu wao, ahadi hii
        inahusu wanadamu wote na kwamba kila mtu amezaliwa katika ulimwengu huu, akiwa
        anatambua kuwa Allah (S.W) ndiye Mola wake na Mungu wa pekee.

        Vikwazo vya kutekeleza ahadi ya utii

        Ingawa mwanadamu ameahidi kumtii na kumwabudu Mola wake lakini kuna nguvu mbili
        zinazosababisha kuasi ahadi yake katika maisha ya kila siku hapa duniani. Nguvu hizo
        ni moja nguvu ya ndani na ya pili ni nguvu za nje ya nafsi yake. Vikwazo hivi aghalabu
        hufanya kazi kwa kushirikiana, ingawa inaweza ikatokea kila kimoja kikafanya kazi peke
        yake. Ufafanuzi wa vikwazo hivyo ni huu ufuatao:

        Kwanza, matamanio ya nafsi. Hiki ni kikwazo kinachotokana na mwanadamu mwenyewe
        nafsini mwake. Mwanadamu ameumbiwa matamanio na akatakiwa apambane nayo ikiwa
        matamanio hayo yanamtoa katika utii. Ieleweke kwamba mwanadamu hana kosa kutamani
        lakini suala ni kwamba anatamani nini? Anatamani yaliyo halali; ndoa, kula, kunywa
        au  kutembea?  Au  anatamani  yaliyoharamishwa;  zinaa,  kamari,  pombe  au  nguruwe?
        Mwanadamu akitamani yaliyo halali, haingii katika uasi wa ahadi kwa sharti la kuwa
        muda unaruhusu. Mfano kula ni halali lakini ikiwa mchana wa Ramadhan haruhusiwi.
        Hivyo, ingawa kuna baadhi ya vitu ni halali lakini achunge vigezo na masharti. Kwa
        upande wa kutamani yaliyo haramu, hii haikubaliki. Katika kutahadharisha kikwazo hiki
        Qur’an inasema:

                                           َ
                                     ً  َ ۡ َ ُ ُ َ َ    َ َ  ُ َ َ ُ َ  َ َ َ  َّ  َ َ ۡ َ َ  َ
                                                         َ
                                                             ٰ
                                                                    ٰ
                                 ٤٣ ليِكو ِهيلع نوكت تنأفأ هىوه ۥههلِإ ذتٱ نم تيءرأ
                                                                           ِ
                Je! Umemwona aliye yafanya matamanio yake kuwa ndio mungu wake?
                Basi je, wewe utakuwa ni wakili wake? (Al-Furqaan, 25:43)
                                                        َ
                                                     َّ
                   ۡ َ  َ  ۡ َ  َ  َ  َ َ َ َ  ۡ  َ  َ  ُ َّ  ُ َ َ ُ َ َ  ُ َ  َ َ َ  َّ  َ َ ۡ َ َ  َ  َ
                                                           ٰ
                                                                  ٰ
                              ٰ
                                            ٰ
                ۦِهبلقو ۦِهِعمس ع متخو ملِع ع للٱ هلضأو هىوه ۥههلِإ ذتٱ نم تيءرفأ
                  ِ
                                       ٖ
                                                                          ِ
                                                             َ
                            َ  ُ  َّ َ َ  َ َ  َ  َّ  ۡ َ  ۡ َ  َ ٗ َ   َ َ  َ  َ َ  َ َ َ
                                                               َ
                                                                           ٰ
                                                                ٰ
                                                 ۢ
                         ٢٣ نوركذت لفأ ِۚللٱ ِدعب نِم ِهيِدهي نمف ةوشِغ ۦِهصب ع لعجو
                                                                      ِ
                                                 232
   237   238   239   240   241   242   243   244   245   246   247