Page 243 - EDK_F5
P. 243

SURA YA TISA                                                   HISTORIA KATIKA UISLAMU

                Je! Umemwona aliye fanya matamanio yake kuwa ndiye mungu wake,
                na Mwenyezi Mungu akamwacha apotee pamoja na kuwa ana ujuzi, na
                akapiga muhuri juu ya masikio yake, na moyo wake, na akambandika
                vitanga  machoni  mwake? Basi nani  atamwongoa huyo  baada ya
                Mwenyezi Mungu? Hamkumbuki? (Al-Jaathiyah, 45:23)
        FOR ONLINE READING ONLY
        Yaani, ewe Mtume! Umemwona huyo mwenye kufanya matamanio yake ndiye mungu
        wake wa kumuabudu, akamnyenyekea, na akamtii, na akaiacha Njia ya Haki na hali anaijua,
        na akaziba masikio yake asisikie waadhi, na moyo wake asiamini Haki, na akabandika
        vifuniko vya macho asione ya kuzingatiwa?  Basi nani wa kumuongoa mtu huyu baada ya
        kwishapuuzwa na Allah (S.W)? Je! Mnaacha kutazama ili msipate kukumbuka?

        Pili, kikwazo cha wazazi au walezi. Kwa kuwa binadamu ni kiumbe kinachoathiriwa
        na mazingira yake, athari hiyo inaweza kuwa mbaya au nzuri. Hivyo, wazazi au walezi
        wanabeba nafasi kuwa katika kumkuza katika wema au uovu mtoto wao. Mitume peke
        yao, ndio hawaathiriwi na mazingira yao, kwa kuwa Mola wao Mlezi amewakinga na
        athari hizo za kimazingira. Imepokewa katika Muwatta Malik (1/393) kuwa:

                “Kila  mtoto  huzaliwa  katika  umbile  la  fitra,  basi  wazazi  wake
                wanamgeuza kuwa Myahudi, au wanamgeuza kuwa Mkristo...”

        Naam, hiyo ndiyo kazi inayofanywa na wazazi au walezi wa mtoto katika kumfanya aasi
        ahadi yake kwa Muumba wake, nacho ni kikwazo cha pili kati ya vikwazo vitatu.

        Tatu, shetani. Shetani ni kikwazo kikubwa katika kumchochea mwanadamu aasi ahadi yake.
        Hii ni kwa sababu shetani ana nguvu mno ukilinganisha na vikwazo vilivyotangulia. Kuna
        shetani wa kijini na wa kibinadamu. Yaani, shetani ni mazingira yote yanayompumbaza
        mwanadamu  katika  kutekeleza  ahadi  yake.  Katika  kitabu  cha  Sharhu  Mushkal  Athar
        (10/5) kuna Hadith Qudsi isemayo:

                Hakika  Nimewaumba waja  Wangu  wote  Hunafaa (wapwekeshaji),
                lakini waliwajia mashetani na wakawatenga na dini yao, wakawakataza
                nilichoruhusu,  wakawamrisha wanishirikishe  na mambo ambayo
                hawana ujuzi nayo.

        Uhusiano wa ahadi ya utii na ahadi nyingine

        Ahadi hii ya utii ina uhusiano na ahadi nyingine zilizotajwa katika aya za Qur’an, ingawa
        kila ahadi ilikuwa na muktadha na wahusika wake. Ahadi hii ya utii iliwahusisha wanadamu
        tu pasi na kiumbe kingine chochote. Allah (S.W) aliahidiana na mwanadamu na kufunga
        mkataba wa kwamba binadamu atatii kila atakaloamrishwa na Mola wake Mlezi wakati
        Mola Mlezi aliahidi kumruzuku kiumbe wake. Ufuatao ni uhusiano wa Ahadi ya Utii na
        ahadi nyingine katika Qur’an:
                                                 233
   238   239   240   241   242   243   244   245   246   247   248