Page 245 - EDK_F5
P. 245

SURA YA TISA                                                   HISTORIA KATIKA UISLAMU

        Kufanana kwao, ahadi hii ya Mitume inafanana na Ahadi ya Utii katika lengo kwani
        ingawa  iliwahusu  Mitume  tu  katika  kufikisha  ujumbe  wa Allah  (S.W)  lakini  ililenga
        kuwakumbusha wanadamu kutekeleza ahadi yao ya utii, jambo ambalo ndilo lengo la
        Ahadi ya Utii. Kutofautiana kwao, zinatofautiana katika wahusika, Ahadi ya Mitume
        iliwekwa baina ya Allah (S.W) na Mitume, wakati Ahadi ya Utii, iliwekwa baina ya Allah
        FOR ONLINE READING ONLY
        (S.W) na wanadamu wote.

        Tatu, Ahadi ya waumini kwa Allah (S.W). Ahadi hii iliwekwa baina ya waumini na Mola
        wao Mlezi. Msingi wake ni kutekeleza mapambano baina ya haki na batili, ili uadilifu
        usimame katika mgongo wa dunia. Qur’an inaliweka wazi hili na kusema:
                                            َ
                  ُ ۡ َ ُ َ ۡ  َ  َ َ  َّ  ُ ۡ َ  ۡ َ َ َّ  ْ  ُ َ َ َ  ْ ُ  َ َ  ٞ  َ  َ  ۡ ُ  ۡ  َ ّ
                                                       ٰ
                            ٰ
                مهنِمو ۥهبن ضق نم مهنِمف ۖ ِهيلع للٱ اودهع ام اوقدص لاجر ينِنِمؤملٱ نِم
                                                                       ِ
                                                             ٗ  ۡ َ  ْ ُ  َّ َ َ َ ُ َ َ  َّ
                                                         ٢٣ ليِدبت اولدب امو ۖرِظتني نم
                Miongoni mwa Waumini wapo watu walio timiza waliyo ahidiana na
                Mwenyezi Mungu. Baadhi yao wamekwisha kufa, na baadhi wanangojea,
                wala hawakubadilisha (ahadi) hata kidogo. (Al-Ahzaab, 33:23)

        Miongoni mwa  Waumini  wapo watu waliomuahidi  Allah (S.W) kuwa watasimama
        imara na Mtume katika vita. Nao wakatimiza ahadi yao. Miongoni mwao wapo walio
        pata  utukufu  wa  kufa  mashahidi,  na  wengine  wamebakia  hai  wakingojea  nao  kupata
        utukufu huo. Wala hawakuigeuza ahadi ya Allah (S.W) waliyoiweka juu ya nafsi zao,
        wala hawakugeuza chochote katika hayo. Kufanana kwao, Ahadi ya Waumini kwa Allah
        (S.W), inafanana na Ahadi ya Utii katika lengo kwani suala la kupambana katika njia ya
        Allah (S.W) ni sehemu ya utii walioahidi wanadamu kuutekeleza katika Ahadi ya Utii.
        Kutofautiana kwao, katika wahusika, Ahadi ya Waumini kwa Allah (S.W), inawahusu
        Waislamu tu wakati Ahadi ya Utii inawahusu wanadamu wote.

        Mazingatio kutokana na ahadi ya utii

        Ahadi ya Utii inaoneshwa kwamba mwanadamu  alimuahidi Allah (S.W) kumwabudu
        Yeye pekee kama Mola wake Mlezi. Ili mtu asisahau ahadi yake, Allah (S.W) ametuma
        Manabii kwa mwanadamu:

                 ۡ َّ  ُ ۡ َ َ ُ َّ  ْ  ُ َ ۡ َ َ َّ  ْ  ُ ُ ۡ  َ  ً  ُ َّ  َّ  ُ  ّ ُ  َ ۡ َ َ ۡ َ  َ  َ
                              ٰ
                نم مهنِمف ۖتوغطلٱ اوبِنتجٱو للٱ اودبعٱ نأ لوسر ٖةمأ ك  ِ ف انثعب دقلو
                                                       ِ
                                                                    ِ
                                                        َ
                  َ  ۡ  َ ْ  ُ  ُ َ  َ  ۡ  ْ  ُ  َ ُ َ َ  َّ  ۡ َ ۡ َّ َ ۡ َّ  ُ ۡ َ ُ َّ  َ َ
                                                ٰ
                فيك اورظنٱف  ِ ضرۡلٱ  ِ ف اويرِسف  ۚةللضلٱ ِهيلع تقح نم مهنِمو للٱ ىده
                                                                  َ  ّ َ ۡ ُ  َ َ َ َ
                                                                        ُ
                                                                              ٰ
                                                             .٣٦ ينبِذكملٱ ةبِقع نك
                                                                    ِ
                Na kwa hakika kwa kila umma tuliutumia Mtume tukasema kwamba:
                Muabuduni Mwenyezi Mungu, na muepukeni Shetani. Basi kati yao
                wapo alio waongoa Mwenyezi Mungu. Na kati yao wapo ambao ulio
                wathibitikia upotovu. Basi tembeeni katika ardhi, muangalie ulikuwaje
                mwisho wa wanao kanusha.(An-Nahl 16:36)
                                                 235
   240   241   242   243   244   245   246   247   248   249   250