Page 244 - EDK_F5
P. 244

SURA YA TISA                                                   HISTORIA KATIKA UISLAMU

        Kwanza, Ahadi ya Amana. Ahadi ya Amana inauhusiano wa karibu na Ahadi ya Utii.
        Hii ni kwa sababu zote zinamkusudia mwanadamu kutimiza lengo la kuumbwa kwake
        ambalo ni kumwabudu Mola wake Mlezi. Katika kujadili hili, aya ya Qur’an, (Ahazab,
        33:72) inasema:

                           ۡ
        FOR ONLINE READING ONLY
                 َ  ۡ َ ۡ  َ  َ َ َ ۡ َ  َ  َ ۡ َ  َ  َ  َ  ۡ  َ  َ  ۡ  َ  َ َ َّ  َ  َ َ َ َ  َ  ۡ  َ ۡ َ َّ
                                                                               َ
                                                          ٰ ٰ
                نقفشأو اهنلِمي نأ ينبأف  ِ لابلٱو  ِ ضرۡلٱو  ِ تومسلٱ ع ةناملٱ انضرع انِإ
                                           ِ
                                               ٗ  ُ َ  ٗ  ُ  َ َ َ  ُ َّ  ُ َ  ۡ  َ َ َ َ َ ۡ
                                                                           َ
                                                                    ٰ
                                          .٧٢ لوهج امولظ نك ۥهنِإ ۖنسنلٱ اهلحو اهنِم
                                                                       ِ
                Kwa hakika Sisi tulikadimisha amana kwa mbingu na ardhi na milima;
                na vyote hivyo vikakataa kuichukua na vikaogopa. Lakini mwanadamu
                akaichukua. Hakika yeye amekuwa dhalimu mjinga. (Al-Ahzab, 33:72)
        Yaani, Sisi kwa hakika tulizitaka  mbingu na ardhi na milima  zichukue amana, nazo
        zikakataa  kuichukua, na wakaiogopa. Lakini  mwanadamu  aliichukua.  Hakika yeye
        amekuwa ni mkubwa wa kujidhulumu nafsi yake kwa kutojua jukumu la kuchukua huko.
        Kufanana kwao, lengo la Ahadi ya Amana linafanana na la Ahadi ya Utii kwani zote
        zinakusudia kumfanya mwanadamu atekeleze lengo la kuumbwa kwake, ambalo ni ibada
        (Ad-Dhariyat, 51:56). Kutofautiana kwao, tofauti zake ni mbili; mosi, Ahadi ya Utii
        ilihusisha mwanadamu na Mola wake tu, wakati Ahadi ya Amana ilihusisha mbingu,
        ardhi, milima na mwanadamu pamoja na Mola wao Mlezi. Pili, maazimio ya Ahadi ya Utii
        yalikuwa ni kwamba mwanadamu kumtii Mola wake Mlezi na Mola Mlezi kumruzuku
        mwanadamu. Wakati maazimio ya Ahadi ya Amana yalikuwa ni mwanadamu kuibeba
        amana na huku viumbe vitamtumikia mwanadamu katika kutekeleza ubebaji wa amana
        aliyoikubali kuibeba.


        Pili, ahadi ya mitume. Hii ni ahadi iliyofungwa baina ya Allah (S.W) na Mitume wake
        wote kwa wanadamu. Allah (S.W) aliifanya ahadi hii kwa Mitume wote, waliotajwa na
        ambao  hawajatajwa  katika  Qur’an. Kuanzia  Nabii Adam mpaka  Mtume  Muhammad
        (S.A.W). (33:7,23)

                  ۡ   َ   َ  ٰ  َ ُ َ َ  َ ۡ  ُّ  َ َ  َ ۡ ُ َ َ  َ ّ َّ  َ  َ ۡ  َ  َ  ۡ
                                                            ٰ
                نبٱ سيِعو سومو ميِهٰربوَإِ  ٖ حون نِمو كنِمو مهقثيِم نۧـيبلنٱ نِم انذخأ ذوَإِ
                                                                   ِ ِ
                 ِ
                                                                             َ
                                                         ٗ َ  ً َ ّ  ُ ۡ  َ ۡ  َ َ َ َ ۡ َ
                                                               ٰ
                                                   .٧ اظيِلغ اقثيِم مهنِم انذخأو ۖميرم
                Na tulipo chukua ahadi kwa Manabii na kwako wewe, na Nuhu na
                Ibrahim na Isa mwana wa Mariamu, na tulichukua kwao ahadi ngumu.
                (Al-Ahzab, 33:7, 23)
        Yaani,  kumbusha  pale  tulipowekeana   ahadi  na  Manabii  wote  waliotangulia  kuwa
        watafikisha  ujumbe  na  kulingania  Dini  iliyo  sawa,  na  wewe  (Muhammad),  na  Nuhu,
        Ibrahim,  Musa, na Isa bin Maryamu;  na tukachukua kwao ahadi  yenye shani kubwa.


                                                 234
   239   240   241   242   243   244   245   246   247   248   249