Page 282 - EDK_F5
P. 282

SURA YA KUMI                                                       HISTORIA YA UISLAMU

        Mtume  Muhammad  (S.A.W)  baada  tu  alipopewa  utume,  alitakiwa  kuufikisha  ujumbe
        huo kwa kuanza na waliomzunguka  kisha auwasilishe kwa ulimwengu mzima. Naye
        hakufanya  ajizi,  kwani hakupumzika  wala  kutumia muda  mwingi  na watu wake wa
        nyumbani. Alisimama  wakati  wote  akiwalingania  watu  juu  ya Allah  (S.W). Aliubeba
        mzigo huo mzito mabegani mwake, na wala hakuutua, pamoja na kuwa ulikuwa ni mzito.
        FOR ONLINE READING ONLY
        Mzigo wa kuwaongoza walimwengu wote, katika hali zote; amani na hofu, raha na karaha
        kwa miaka ishirini na tatu.
        Mchakato  wa ulinganiaji  wakati  wa Mtume Muhammad (S.A.W) umegawika  katika
        vipindi viwili: Kipindi cha Makka, kilichochukua miaka kumi na tatu na  Kipindi cha
        Madina, kilichochukua miaka kumi. Kila kimoja kati ya vipindi hivyo, kilikusanya awamu
        tatu; kila awamu ilikuwa na mambo yaliyokuwa tofauti na awamu nyingine. Kwanza,

        kipindi cha Makka kilikuwa na; (i) Awamu ya da’awa ya siri, ilidumu katika miaka mitatu
        ya mwanzo ya utume. (ii) Awamu ya da’awa kwa watu wa Makka iliyoanza mwaka wa
        nne mpaka mwaka wa kumi wa utume. (iii) Awamu ya da’awa nje ya Makka, iliyoanza
        mwishoni mwa mwaka wa kumi wa utume mpaka kabla ya Hijra ya Madina. Pili, kipindi

        cha Madina nacho kilikuwa na awamu tatu; (i) Awamu ya kustawisha hali za Waislamu
        na miundombinu ya Madina, hii ilihusisha miaka ya mwanzo ya Hijra (ii) Awamu ya
        kupambana na udhalimu wa washirikina wa Makka, Wayahudi na Wanafiki wa Madina.
        (iii) Awamu ya kupambana na udhalimu wa dola za Kirumi na Kiajemi, hii ilianza mwaka
        wa saba hadi Mtume Muhammad (S.A.W) alipotawafu.

        Njia alizotumia Mtume Muhammad (S A W) Kulingania Uislamu na
        Hekima Zake


         Kazi ya 10 6
         Shirikiana na wanafunzi wenzako kusoma aya na tafsiri yake, kisha bainisha mambo
         makubwa  manne yanayotajwa katika aya hiyo

                                                                 َ
                    َ ْ َ ْ    ُّ َ ْ  َ  ْ ْ َ  َ َ  ًّ َ  َ ْ  ُ َ ْ َ ْ ُ َ ْ  َّ  َ  َ ْ  َ َ  َ
                    كِلوح نِم اوضفنل بلقلا ظيِلغ اظف تنك ولو ۖ مهل ت ِ لن ِللا نِم ٍةحر امبف
                                      ِ
                                                                                     ِ
                                                                 َ
                   َّ  َّ  َ  َ ْ َّ َ  َ ْ َ َ َ َ  ْ  َ ْ  ْ ُ ْ  َ ْ ُ ْ  ْ َ ْ َ ْ ُ ْ َ  ُ ْ َ
                                َ َ
                                                             َ
                  نِإ ۚ ِللا ع كوتف تمزع اذإف ۖ رملا  ِ ف مهرواشو مهل رِفغتساو مهنع فعاف ۖ
                                            ِ
                                               ِ
                                                          ِ
                                                                       َ  ّ  َ َ ُ  ْ  ُّ  ُ َّ
                                                                                    َ
                                                                   ١٥٩ ينِ ِ كوتملا بِي للا
                 Basi ni kwa sababu ya rehema itokayo kwa Mwenyezi Mungu ndio
                 umekuwa  laini  kwao.  Na  lau  ungeli  kuwa  mkali,  mwenye  moyo
                 mgumu, bila ya shaka wangelikukimbia. Basi wasamehe, na waombee
                 maghfira, na shauriana nao katika mambo. Na ukisha kata shauri basi
                 mtegemee  Mwenyezi  Mungu.  Hakika  Mwenyezi  Mungu  huwapenda
                 wanaomtegemea. (Al-Imran, 3:159).
                                                 272
   277   278   279   280   281   282   283   284   285   286   287