Page 284 - EDK_F5
P. 284

SURA YA KUMI                                                       HISTORIA YA UISLAMU

            e)  Kuchukia maovu na kujitenga pangoni katika pango la Hira ili kutafuta msaada wa

               Allah (S.W) wa namna ya kuikomboa jamii kutokana na dhulma.

        Aidha, Mtume Muhammad (S.A.W) alipewa mafunzo  mahususi  kupitia Qur’an kama
        ifuatavyo:
        FOR ONLINE READING ONLY

            a)  Ambapo katika wahyi wa kwanza; aliamrishwa asome kwa ajili ya Mola wake
               (‘Alaq, 96:1-5) na wahyi uliofuatia  unaopatikana  katika  suratul Muzzamil,
               Muddathir na Qalam Mtume Muhammad (S.A.W) aliamrishwa kuswali usiku,

               kusoma Qur’an kwa mazingatio, kumtaja Allah (S.W) kila wakati na kunyenyekea
               kwake, kumtegemea Allah (S.W), kuwa na subira, kusafisha nguo, kupuuza mabaya,
               kufanya ihsan kwa ajili ya kutafuta radhi za Allah (S.W)- Rejea Muzzammil, 73:1-
               10) na (Muddathir,74:1-7).


        Maandalizi haya yalimfanya awe na tabia njema kiasi cha kuweza kumvutia mtu yeyote
        aliyekutana naye. Allah (S.W) anampongeza kupitia Qur’an kwa kusema: “Na hakika
        wewe una tabia tukufu.” (Qalam, 68:4).


        Kuwaunganisha  Answari na Muhajirina, Muhajirina  walikuwa pamoja  na Mtume
        Muhammad  (S.A.W) kwa muda  wa miaka  kumi  na tatu,  hivyo, walikuwa  wamepata
        mafundisho ya kutosha kuhusu Uislamu, wakati  Answari walikuwa wapya katika

        Uislamu. Hivyo, Mtume Muhammad (S.A.W) alitumia fursa hiyo kuwaunganisha baina
        ya makundi hayo mawili ili Muhajirina wawasomeshe Answari mambo yanayohusiana
        na Uislamu wao. Aidha, aliwaunganisha mtu mmoja kutoka Answari na mmoja kutoka
        Muhajirina na kuwafanya kuwa ndugu wa kiimani baina yao. Lengo ni kufuatiliana kwa

        ukaribu ili kila mmoja anufaike na neema alizokuwa nazo ndugu yake, ikiwemo elimu na
        mali. Udugu huo ulifanywa kama wa damu. Ikawa kuko kurithiana baina yao kwa sudus
        (1/6), mpaka ilipokuja kufutwa sharia hii.
                               َ
                                                                           ۡ
                      َ
                ۡ ُ ُ َ ۡ ُ ُ َ ۡ ۡ َ َ َ َ  َّ  َ  َ ُ َ  ۡ  َ  ۡ  َ  َ َ  ۡ  َ َ  َ َّ َ  َ َ َ َ َ  ّ ُ  َ
                            ٰ
                                                                      ٰ
                                                          ٰ
                مهوتأـف مكنميأ تدقع نيِلٱو ۚنوبرقلٱو نا ِ لدولٱ كرت امِم لوم انلعج كِلو
                                                       ِ
                                                                      ِ
                                                                                ٖ
                                                 ً   َ  ۡ  َ ّ ُ َ ٰ  َ َ َ  َ َّ  َّ  ۡ ُ َ  َ
                                            .٣٣ اديهش ٖءش ك ع نك للٱ نِإ ۚمهبي ِ صن
                                                   ِ
                                                            ِ
                Na kila mmoja tumemwekea warithi katika waliyoyaacha wazazi wawili
                na jamaa. Na mlio fungamana nao ahadi wapeni fungu lao. Hakika
                Mwenyezi Mungu ni Shahidi wa kila kitu, (Nisaa, 4:33).
        Mfano mzuri wa kuunganishwa watu wawili wawili baina ya Answari na Muhajirina ni
        Abdur Rahman bin Auf aliyekuwa muhajiri aliyefanywa kuwa ndugu wa Saad aliyekuwa
                                                 274
   279   280   281   282   283   284   285   286   287   288   289