Page 283 - EDK_F5
P. 283

SURA YA KUMI                                                       HISTORIA YA UISLAMU

        Mtume Muhammad (S.A.W) alitumia njia mbalimbali za kufikisha ujumbe ili kufanikisha

        lengo la kutumwa kwake kwa walimwengu, miongoni mwa njia hizo ni:

        Kulingania kwa siri: njia hii ndio msingi wa ulinganiaji wa Mtume Muhammad (S.A.W),
        alianza  kulingania  familia  yake,  kisha  rafiki  zake  na  jamaa  zake  wa  karibu. Alikuwa
        FOR ONLINE READING ONLY
        anakutana  nao kwa siri mmoja mmoja;  kwa njia hii walisilimu  watu kama Abubakar

        (R.A) aliyekuwa rafiki yake, Ali bin Abi Talib (R.A) mtoto wa ami yake, Khadija binti
        Khuwailid (R.A) mke wake na Zaid bin Harith (R.A) mtumishi wake wa ndani. Hao
        ni watu wa mwanzo kusilimu, waliokuwa karibu mno na Mtume Muhammad (S.A.W).
        Pia, aliendelea kutumia njia hii ya siri na kufanikiwa kupata kundi la watu zaidi ya 40

        na kuamua kuwapa mafunzo kuhusu Uislamu katika nyumba ya Bwana Arqam bin Abi
        Arqam.

        Kutoa hotuba hadharani: Mtume Muhammad (S.A.W) alipoamrishwa na Mola wake
        atangaze ujumbe wa Uislamu kwa jamii nzima kupitia Qur’an (Hijri, 15:94 na Shuaraa,

        26:214-217) alipanda juu ya mlima Safa akapiga mbiu ya dharura, kuziita koo zote za
        Kiqureshi kwa majina yao. Baadaye, akatoa hotuba na kueleza lengo la kutumwa kwake
        kwa walimwengu, ingawa hawakumkubali na Abu Lahab akamuapiza, ndio Allah (S.W)
        akamlani kama ilivyobainisha katika Qur’an (Surat Lahab, 111:1-3).


        Kuishi kwa tabia njema, Mtume  Muhammad  (S.A.W) alikuwa  hana  mpinzani  kwa
        tabia njema katika maisha yake. Alikuwa na tabia zilizomvutia kila aliyeamiliana naye.
        Hii ilitokana  na maandalizi aliyoyapata  kabla  na wakati  wa kupewa utume.  Mtume
        Muhammad (S.A.W) aliandaliwa bila ya kujijua kabla ya kupewa utume, maandalizi haya

        yanajulikana kama maandalizi ya Ki-ilham; miongoni mwa maandalizi hayo ni:
            a)  Kuzaliwa katika kabila la Qureysh katika kizazi cha Nabii Ibrahim (A.S) kupitia
               kwa Nabii Ismail (A.S);

            b)  Kupewa jina la Muhammad lenye maana sawa na jina la Ahmad lililotabiriwa
               katika Injili;


            c)  Malezi bora aliyoyapata kutoka kwa mama yake mzazi Amina, mama yake wa
               kunyonya Halima, babu yake Abdul-Muttalib na ami yake Abu Talib;


            d)  Ndoa ya Mtume Muhammad (S.A.W) na Bi Khadija (R.A) ilikuwa ni mpango wa
               Allah (S.W) ili kumtajirisha Mtume Muhammad (S.A.W) kupitia mkewe huyo,
               baadaye mali yake ikatumikia jamii ya Kiislamu; na


                                                 273
   278   279   280   281   282   283   284   285   286   287   288