Page 286 - EDK_F5
P. 286

SURA YA KUMI                                                       HISTORIA YA UISLAMU


                                                              َ
                 َ ۡ َ ۡ  ْ  ُّ َ  َ  ۡ ۡ َ  َ َ  ًّ َ  َ  ُ َ ۡ َ ۡ ُ َ  َّ  َ ّ َ ۡ  َ َ  َ
                ۖكِلوح نِم اوضفنل بلقلٱ ظيِلغ اظف تنك ولو ۖمهل ت ِ لن ِللٱ نِم ٖةحر امبف
                                                                                  ِ
                                   ِ
                                                              َ
                َّ  َّ  َ  َ ۡ َّ َ  َ ۡ َ َ َ َ  ۡ  َ  ۡ  ۡ ُ ۡ  َ  َ ۡ ُ ۡ  ۡ َ ۡ َ ۡ ُ ۡ َ  ُ ۡ َ
                             َ َ
                نِإ ِۚللٱ ع كوتف تمزع اذإف رملٱ  ِ ف مهرواشو مهل رِفغتسٱو مهنع فعٱف
                                                       ِ
                                         ِ ِۖ
                                                                    َ  ّ  َ َ ُ  ۡ  ُّ  ُ َّ
                                                                                 َ
                                                               .١٥٩ ينِ ِ كوتملٱ بِي للٱ
        FOR ONLINE READING ONLY
                Basi ni kwa sababu ya rehema itokayo  kwa Mwenyezi  Mungu ndio
                umekuwa laini kwao. Na lau ungeli kuwa mkali, mwenye moyo mgumu,
                bila ya shaka wangeli kukimbia. Basi wasamehe, na waombee maghfira,
                na shauriana nao katika mambo. Na ukisha kata shauri basi mtegemee
                Mwenyezi Mungu. Hakika Mwenyezi Mungu huwapenda wanao
                mtegemea, (Al-Imran, 3:159).

        Kutatua changamoto za jamii, Mtume Muhammad (S.A.W) alikuwa hajisikii vyema
        kama kuna mtu yeyote katika wafuasi wake au jamii kwa ujumla anasumbuka na tatizo,
        alililazimisha kumsaidia au kuwa sababu ya kulitatua tatizo lile. Qur’an inaweka bayana
        hilo kwa kusema:


                     َ
                                           َ
                                                                             ٓ
                  ُ ۡ َ   ٌ   َ ۡ ُّ َ  َ  ۡ َ ٌ  َ ۡ ُ    ُ  َ  ۡ ّ  ٞ  ُ َ ۡ ُ َ َ ۡ َ  َ
                مكيلع صيرح متِنع ام ِهيلع زيزع مكِسفنأ نِم لوسر مكءاج دقل
                                                ِ
                            ِ
                                                                ٞ  َّ  ٞ  ُ َ َ  ۡ ُ  ۡ
                                                           .١٢٨ ميِحر فوءر ينِنِمؤملٱب ِ
                Hakika amekwishakujieni Mtume kutokana na nyinyi wenyewe;
                yanamhuzunisha yanayokutaabisheni; anakuhangaikieni sana. Kwa
                Waumini ni mpole na mwenye huruma. (Taubah,9:128).

        Kubashiri na kuonya: Hii ni njia waliyoitumia Mitume wote kwani ndio lengo hasa
        la kuletwa Mitume duniani. Mtume Muhammad (S.A.W) mara kwa mara aliwabashiria
        Maswahaba zake mambo mazuri kama vile waliotenda  mema kwa kiwango cha juu
        aliwabashiria  Pepo, mfano mzuri  ni Maswahaba kumi  waliobashiriwa  Pepo.  Aidha,
        alionya tabia mbaya kwani matokeo yake ni Motoni. Qur’an inathibitisha hili kwa kusema:

                                                   ۡ
                                 ٗ َ  َ ٗ ّ َ ُ  َّ  َ َ َ ۡ  َ  ٓ  َ َ  َ  َ ّ  َ  ۡ  َ ُ َ َ ۡ  َ  ّ  َ ۡ  َ
                                                              َ
                                                  ٰ
                                                                        ٰ
                            .١٠٥ اريِذنو ا ِ شبم لِإ كنلسرأ امو  ۗلزن قلٱبو هنلزنأ قلٱبو
                                                                    ِ
                                                                              ِ
                                                                                  ِ
                                                                ِ
                Na kwa Haki tumeiteremsha, na kwa Haki imeteremka. Na hatukukutuma
                ila uwe mbashiri na mwonyaji. (Israa, 17:105).
        Kuwa mfano mwema  wa kuigwa:  Mtume  Muhammad  (S.A.W) alikuwa  mfano  wa
        kuigwa katika kila kipengele cha maisha yake. Hii ni kwa sababu alivaa kofia za watu
        wote mbele ya macho ya Maswahaba wake. Alikuwa mwalimu kwani aliwafunza, alikuwa
        daktari kwani aliwatibu, alikuwa askari kwani alisimamia sheria katika kulinda uhai na
        mali zao, alikuwa mshauri kwani aliwapa ushauri nasaha, alikuwa mlezi kwani aliwalea,
                                                 276
   281   282   283   284   285   286   287   288   289   290   291