Page 285 - EDK_F5
P. 285

SURA YA KUMI                                                       HISTORIA YA UISLAMU

        Answari. Pia, Salman Faris aliyechukuliwa kama muhajiri kwa kuwa hakuwa na asili ya
        Madina wala Makka, aliunganishwa udugu na Abu Dardaa aliyekuwa Answari. Hawa na

        wengine walitumia muda mwingi kuelemishana kuhusu dini yao na kusaidiana katika
        maisha yao yote.
        FOR ONLINE READING ONLY
        Kufunga mikataba:  mikataba  iliwezesha  kufikisha  ujumbe  wa  Uislamu  wakati  wa
        Mtume  Muhammad  (S.A.W) kwani  ilisaidia  uhusiano  mzuri  baina  ya waumini  wao

        kwa wao na hata wao na wasiokuwa Waislamu. Mfano wa mikataba iliyotumika katika
        kulingania ni Mikataba miwili ya Aqaba, Mkataba wa Hudaibiya, na Mkataba wa Madina.
        Kupitia mikataba hii watu walisilimu na wengine kuona uzuri wa Uislamu. Mfano, Qur’an
        inasimulia vipengele vya mkataba wa wanawake walio hajir kwenda Madina.

                                                                                 َ
                 َ  َ ٗ ۡ َ  َّ  َ  ۡ  ۡ ُ  َّ  َ  َ  َ َ َ ۡ َ ُ ُ َ ۡ ُ  ۡ  َ َ َ  َ  َّ  َ ُّ َ
                                                                  ٓ
                                          ٰٓ
                                                                          ُّ
                                                         ٰ
                                                                                  ٰٓ
                لو أـيش ِللٱب نكشي ل نأ ع كنعيابي تنِمؤملٱ كءاج اذِإ بلنٱ اهيأي
                            ِ
                                                  ِ
                                ِ
                                                                          ِ
                                                         َ
                      َ
                                                            ۡ
                                                        َ
                 َّ  ۡ َ ۡ َ ُ َ َ ۡ  َ  َ ۡ ُ َ  ۡ  َ  َ  َ َّ ُ َ ۡ َ ُ ۡ  َ  َ  َ َ ۡ َ  َ  َ َ  ۡ  ۡ َ
                                                       ٰ
                                     ٰ
                نهيِديأ ينب ۥهنيتفي نتهبب ينِتأي لو نهدلوأ نلتقي لو ينِنزي لو نقسي
                  ِ
                                        ِ
                                                                                ِ
                               ِ
                                    ٖ
                                   َ
                ٞ ُ َ  َ َّ  َّ َ َّ  َّ ُ ۡ  ۡ َ ۡ َ َّ ُ ۡ َ  َ  ُ ۡ َ  َ َ  ۡ َ  َ  َ َّ  ُ ۡ َ َ
                روفغ للٱ نِإ ۚللٱ نهل رِفغتسٱو نهعيابف  ٖ فورعم  ِ ف كني ِ صعي لو نهِلجرأو
                                                 ِ
                                                                              ِ
                                                                               ٞ   َّ
                                                                           .١٢ ميِحر
                Ewe Nabii! Watakapokujia wanawake Waumini wanakuahidi ya kwamba
                hawatamshirikisha  Mwenyezi  Mungu na chochote,  wala  hawataiba,
                wala hawatazini, wala hawatawauwa watoto wao, wala hawataleta
                uzushi wanao uzua tu wenyewe baina ya mikono yao na miguu yao, wala
                hawatakuasi katika jambo jema, basi peana nao ahadi, na uwatakie
                maghfira kwa Mwenyezi Mungu. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwingi
                maghfira, Mwenye kurehemu, (Mumtahina, 60:12).
        Kuwa mpole kwa wafuasi wake: Mtume Muhammad (S.A.W) hakuishi kwa ukali na
        wafuasi wake, hata iweje aliwavumilia na kuwachukulia mapungufu yao ya kibinadamu.
        Mfano, katika vita vya Uhud kuna Maswahaba 50 waliowekwa katika mlima na kupewa
        amri ya kutoshuka, ila kwa amri nyingine ya Mtume Muhammad (S.A.W), lakini wao
        walishuka, walipoona  Waislamu wanakaribia  kushinda. Hapo ushindi ukabadilika,
        kutoka kwa Waislamu ukenda kwa Washirikina, Waislamu 70 wakafa shahidi, Mtume
        Muhammad (S.A.W) akajeruhiwa meno yake, lakini yeye hakuwakaripia, aliwasamehe
        na kuwaombea msamaha  kwa Allah  (S.W). Jambo hili  liliwafanya  watu wanaosilimu
        kutotamani kutoka katika Uislamu. Qur’an inasimulia tukio hili:




                                                 275
   280   281   282   283   284   285   286   287   288   289   290