Page 162 - EDK_F5
P. 162

SURA YA TANO                                                           KUFASIRI QUR’AN

        Nne, pia  wanazuoni  wa zama  za  Tabiin,  walijiepusha  sana  kufafanua  aya  fiche
        (Mutashabihat) katika Qur’an.

        Tafsir ya Qur’an katika zama zilizofuata


        Historia ya tafsir  ya Qur’an katika zama zilizofuata (baada ya Tabiin), ilishuhudia juhudi
        FOR ONLINE READING ONLY
        mbalimbali zilizofanywa na kuendelezwa kimaandishi, kutoka katika misingi iliyowekwa
        na watangulizi wao. Kipindi hiki kinagawanyika katika hatua nne zifuatazo:

        Hatua ya kwanza, Muhaddithun (Wanazuoni wa Hadith) kama vile Shu’bah ibn Hajaj,
        aliyefariki  mwaka  160H/  782  M, Waki’i  ibn  Jar’rah  aliyefariki  mwaka  197H/  819M.
        Katika juhudi zao, walikuwa wakijumuisha simulizi mbalimbali za tafsir za aya za Qur’an,
        zilizonasibishwa na Mtume Muhammad (S.A.W) au Maswahaba zake au Tabiiin.

        Hatua ya pili, katika juhudi zilizofanywa baadae (baada ya Tabiin), kuhusu tafsir  ya
        Qur’an, ilikuwa ni kupangwa kwa  tafsir. Katika hatua hii  tafsir mbalimbali  za aya

        zilipangwa na kuandikwa kwa kutenganishwa na Hadith, zikiwa pamoja na silsila ya
        wasimulizi wake (Sanad). Miongoni mwa wanazuoni waliojitokeza katika kuifanya kazi
        hiyo, ni pamoja na Ibn Jarir Twabari aliyefariki mwaka 310H na mwishoni mwa zama hizi
        alijitokeza Abu-Bakr Ibn Mardawah, aliyefariki mwaka 410H.

        Hatua ya tatu, katika  tafsir   ya Qur’an, ilitegemea  vyanzo vyote walivyotumia
        watangulizi  wao (Tabii  tabiin), pamoja  na simulizi  ambazo  miongoni  mwao zilikuwa

        sahihi na zisizo sahihi (Hadith dhaifu), na wakaondoa silsila ya wapokezi. Kwa maana
        katika uandishi, walikuwa wakieleza maoni ya watangulizi wao, bila kuwataja kuwa wao
        ndio waliosema na waliyatoa wapi. Kwa sababu hiyo, zikaenea simulizi nyingi za watu
        wa kitabu (Israiliyat) katika Tafsir walizoandika.

        Hatua ya nne, Tafsir ilitegemea sana ushawishi wa mfasiri na taaluma aliyokuwanayo,

        aina ya kipawa chake na madhehebu yake. Mambo hayo yalishawishi sana tafsir hadi
        ikaenda mbali zaidi katika fani ndogondogo za lugha, ambazo mfasiri amebobea. Mwendo
        huu wa tafsir ndio uliondelea hadi sasa.

         Zoezi la 5 1

             1.  Onesha uhusiano baina ya tafsir, taawil na tarjama
             2.  Kwanini tunahitaji tafsir ya Qur’an?
             3.  Bainisha sababu nne zilizopelekea Tabi’in kujiepusha kufasiri aya Mutashabihat
             4.  Fafanua dhana ya tarjama na namna inavyotofautiana na tafsir




                                                 152
   157   158   159   160   161   162   163   164   165   166   167