Page 164 - EDK_F5
P. 164

SURA YA TANO                                                           KUFASIRI QUR’AN

        Sifa za tafsir Bil Maathur


        Tafsir Bil Maathur ni bora kuliko ngazi zote za tafsir kwa kuwa:
           a) inazingatia ufafanuzi kutoka katika vyanzo vya msingi visivyo na wasiwasi wa

               upogo;
        FOR ONLINE READING ONLY
           b)  inabainisha aya za Qur’an zilizo jumla (mujmal) kwa kutumia aya zingine  zilizo
               wazi au mahususi (mubayyan);

           c)  inabainisha aya  zilizoachwa huru (mutlaq) kwa zingine zilizofungwa (muqayyad);

           d)  inabainisha aya za Qur’an zilizo na maelekezo ya jumla (‘amm) kwa zingine zilizo
               na maelekezo mahususi (khas);

           e)  inaondoa changamoto inayoonesha kuwepo kwa kukinzana baina ya aya moja ya
               Qur’an na nyingine;
           f)  inafafanua vema na kutofautisha baina ya aya zinazofuta (Nasikh) na aya zilizofutwa

               (Mansukh);
           g)  inabainisha  maelekezo  mbalimbali  ya  kisharia  yaliyopo  katika  baadhi  ya  aya

               (Aayat Ahkam), ambazo  hazina  ufafanuzi. Kama vile  aya zinazoeleza  twahara,
               Funga, Zakat na Hijja; na
           h)  inaangalia ufafanuzi uliotolewa katika Sunnah, athari za maswahaba na historia,
               ambayo baadaye ilikuja  kutambuliwa kama sababu ya kuteremshwa kwa aya

               husika.
        Udhaifu katika tafsir Bil Maathur


        Pamoja na ubora usio na shaka wa ngazi hii ya Tafsir, lakini bado wanazuoni walibaini
        udhaifu katika baadhi ya maeneo, hasa ikizingatiwa  upana wa maudhui ya Qur’an,
        yanayoenea  kila nyanja ya maisha na katika mazingira  yote. Miongoni mwa nukta

        zinazoonyesha udhaifu  katika ngazi hiyo ya Tafsir ni pamoja na:

            (a) Mwanzoni, Tafsir Bil Maathur ilisomeshwa kama sehemu ya fani ya Hadith kabla

                haijatenganishwa, hivyo ilizingatia pia vigezo vya isnad na matin kama Hadith.
                Kwa sababu hiyo, haiwezi kukosa kasoro kabisa kwa kuwa katika Hadith pamoja
                na kuwepo kwa vigezo hivyo bado zinabainika Hadith Sahihi, Hasan na Dhaifu
                pia, bali hata Maudhuu. Kwa kuwa tafsir hii ilipita katika njia hizo bila shaka
                simulizi zake hazitakosa madaraja hayo.




                                                 154
   159   160   161   162   163   164   165   166   167   168   169