Page 168 - EDK_F5
P. 168

SURA YA TANO                                                           KUFASIRI QUR’AN

        ya sababu au chanzo. Na neno Nuzul lina maana ya kuteremshwa au kushushwa. Hivyo
        Sababun Nuzuul kwa ujumla  wake ni  somo linalohusu  sababu za  kuteremshwa  kwa
        aya  mbalimbali  za  Qur’an; au ni ujuzi  kuhusu matukio fulani  ya kihistoria,  ambayo
        yanahusishwa na kushuka kwa ibara, sura  au aya fulani za Qur’an.

        Umuhimu wa Sababun nuzuul
        FOR ONLINE READING ONLY
        Haiwezekani kuwa na maarifa ya kufasiri aya za Qur’an vilivyo, bila kujishughulisha na
        simulizi au maelezo yanayoeleza sababu ya kushuka kwake. Hivyo, kufahamu kuhusu
        Sababun Nuzuul kunasaidia kuelewa vema mazingira ambayo aya husika ilishuka. Kwa
        kujua mazingira ya kushuka, inatoa nafasi kwa mfasiri kujua kuwa aya hiyo, ilimaanisha
        nini na kutoa mwongozo wa kuifafanua na kujua matumizi yake mengine, katika hali
        tofauti.
        Kwa ujumla, ujuzi wa Sababun nuzuul unamsaidia mtu  kwanza kuelewa; maana ya
        moja kwa moja na ya kiutendaji kwa kuwa itajibainisha kutoka katika mazingira halisi.
        Pili, sababu inayojitokeza katika kushuka kwa aya huwa inakuwa na hukumu ya kisharia.
        malengo halisi ya aya, kujua kama aya hiyo ni ya jumla au ni mahususi katika matumizi,
        na  katika  mazingira  gani  inapaswa  kutumika.  Vilevile,  kujua  mazingira  ya  kihistoria
        wakati wa Mtume Muhammad (S.A.W) na maendeleo ya jamii ya Kiislamu.

        Kujulikana kwa Sababun nuzuul
        Sabubun nuzuul zinazofahamika na kuaminiwa  ni zile zilizosimuliwa  na Maswahaba
        wa Mtume Muhammad (S.A.W). Aidha, zimechukuliwa pia simulizi zilizothibitishwa
        kwa usahihi, kwa kuzingatia  njia  za usahihishaji  wa Hadith. Miongoni mwa vigezo
        vilivyoangaliwa ni kuwa msimulizi wa sababu hiyo, awe ni katika watu waliokuwepo

        katika eneo ambalo aya husika ilishuka. Ama, simulizi kutoka kwa Tabi’in pekee, ambayo
        haina  muunganiko  na  Swahaba  inadhoofishwa.  Hivyo,  hayakubaliki  maoni  binafsi  ya
        mtu yoyote kusemea kuwa aya fulani ilishuka kwa sababu fulani bila sanad iliyonyooka
        inayomkuta Mtume Muhammad (S.A.W).

        Aina za Asbabun nuzuul
        Asbabun nuzuul ni wingi wa sababun nuzuul. Kuna aina tatu za Asbaabun nuzuul katika

        aya za Qur’an ambapo ya kwanza ni kubainisha au kujibu matukio au hali ya jumla
        iliyojitokeza. Pili, kujibu swali liloulizwa au hoja iliyoibuliwa na mtu au watu, na tatu ni
        sababu nyinginezo tunazozijua na tusizozijua.
        Kwanza, katika sababu ya kubainisha au kujibu matukio au hali iliyojitokeza katika jamii
        kuna mifano mingi ikiwemo:

        Tukio la Abu Lahab; kama anavyosimulia Ibn Abbas (R.A) kuwa Mtume Muhammad

        (S.A.W) alitoka akielekea Al-Batha kisha akapanda mlima na kunadi “Enyi ndugu zangu;
        mara Maquraysh wakakusanyika na kumuelekea. Kisha akasema: “Ikiwa nitawaambia
                                                 158
   163   164   165   166   167   168   169   170   171   172   173