Page 169 - EDK_F5
P. 169

SURA YA TANO                                                           KUFASIRI QUR’AN

        kuwa nyuma  ya mlima  huu kuna maadui  wanakuja kuwashambulia  asubuhi au jioni
        mtaniamini..?  Wakajibu  Maquraysh:  “Ndio”  basi  akasema  kuwaambia  kuwa  “Hakika

        mimi ni mjumbe wa Allah (S.W) nimekuja kuwaonya na adhabu zake kali”. Akasema
        Abu Lahab: “hivi ni kwa sababu hii kweli ndio umetukusanya hapa..? Uangamie kabisa
        FOR ONLINE READING ONLY
        ewe Muhammad..! kwa sababu hii Allah (S.W) akateremsha “Imeangamia mikono ya
        Abu Lahab...” Surat Lahab, 111:1. Hadith imenukunuliwa na Imam Bukhari, VI, Na. 496.

        Surat Lahab ilishuka kwa sababu ya tukio hili, baada ya Abu Lahab kubeza ujumbe wa
        Mtume Muhammad (S.A.W) wazi wazi na kumtamkia maneno ya kumlaani mbele ya
        kadamnasi. Hivyo, Allah (S.W) akamtakasa Mtume wake (S.A.W) na kumrudishia laana
        yake Abu Lahab.


        Tukio la  Sa’i;
        Kabla ya kusilimu Answar walikuwa wanahirimia ibada ya Hija kwa kuwataja masanamu
        yao ambayo waliyaweka katika eneo la Mushallali. Baada ya kusilimu wakaona vibaya
        kwenda Sa’i kati ya Safa na Marwa kwa kuchelea utajo wa masanamu yaliyokuwepo

        kabla ya kusilimu.
        Kwa sababu ya wasiwasi huo Allah (S.W) akateremsha aya ifuatayo:

                                                                         ْ
                   َ
                  ْ َ َ َ ُ  َ َ  َ َ َ ْ  َ  َ ْ َ  ْ  َّ َ ْ َ  َ  َّ  ٓ َ  َ َ ْ َ َ  َ َّ  َّ
                                                              َ
                 ِهيلع حانج لف رمتعٱ وأ تيلٱ جح نمف ۖ ِللٱ رئاعش نِم ةورملٱو افصلٱ نِإ
                                                           ِ ِ
                                      ِ
                                    ٌ  َ  ٌ  َ َ َّ  َّ َ  ً ْ َ َ  َّ َ َ  َ َ  َ  َ  َّ َّ َ  َ
                                 ١٥٨ ميِلع رِكاش للٱ نإف اۭيخ عوطت نمو ۚ امهب فوطي نأ
                                                                         ِ ِ
                                                    ِ
                Hakika Safa na Marwa ni katika ishara za Allah (S.W)...
                (Al-Baqara, 2:158).
        Pili, katika sababu ya kubainisha au kujibu matukio au hali iliyojitokeza katika jamii kuna
        mifano mingi ikiwemo:

        Swali kwa Mtume Muhammad (S A W) kuhusu mali; kuna matukio mengi ambapo
        Mtume Muhammad (S.A.W) aliulizwa  na Maswahaba zake (R.A) kuhusu Akida, na
        hukumu mbalimbali za Kiislamu. Miongoni mwa waliyowahi kumuuliza na ukashuka
        wahyi kubainisha ni swali la Swahaba Jabir (R.A) kama anavyosimulia katika Hadith
        iliyopokelewa na Imam Bukhar kuwa: Anasimulia Jabir (R.A) kuwa: Mtume Muhammad
        (S.A.W) na Abu Bakr (R.A) walikuja  kwa mguu kuja kuniona  nilipokuwa  nikiumwa
        katika  makazi  ya  Banu  Salama.  Mtume  Muhammad  (S.A.W) akanikuta  nikiwa
        nimezirai, akaomba maji na kutia udhu, na kutoka katika maji yale akanirushia matone.
        Nikazinduka na kusema “Ewe Mtume wa Allah (S.A.W)..! Unaniamrisha kufanya nini
        katika mali yangu..? Hapo hapo ikashuka aya katika Surat Nisaa, 4:11 kuwa “Allah (S.W)
        anakuamrisheni kuhusu urithi kwa watoto...” (Bukhar, VI, Na.101). Aya hiyo ilishuka

                                                 159
   164   165   166   167   168   169   170   171   172   173   174