Page 165 - EDK_F5
P. 165

SURA YA TANO                                                           KUFASIRI QUR’AN

            (b) Katika Tafsir Bil Maathur, ufafanuzi wa baadhi ya aya  wafasiri wanatofautiana
                katika kubainisha sababu za kushuka kwa aya.
            (c) Ngazi hii ya  Tafsir hapo mwanzoni ilibainika  kuwa na simulizi   za kiyahudi

                na kikristo zilizochanganywa  ndani yake.  Hata hivyo, baadaye  wanazuoni
        FOR ONLINE READING ONLY
                walibainisha  na kuzitambulisha  kwa jina  la  Israiliyat. Ibn Khaldun mmoja
                kati ya wanazuoni hao, anasema katika kitabu chake Mukaddima kuwa; wengi
                katika Wayahudi  wa Yemen  walioingia  katika  Uislamu  walitoka  katika  kabila
                la  Himyar. Walipoingia  katika  Uislamu,  bado walibaki  na  taarifa  walizozipata

                katika Uyahudi, kama vile habari za mwanzo wa uumbaji, matukio yaliyotabiriwa
                kutokea hapo baadaye. Taarifa hizo hazikuwa na uhusiano wa moja kwa moja na

                Uislamu. Miongoni mwao walikuwemo Ka’ab ibn Ahbar na Wahb ibn Munabbih
                na wengineo. Ufafanuzi waliotoa katika kusherehesha Qur’an ulikuwa na athari
                ya simulizi hizo.

        Tafsir Bil Ray


        Ngazi ya pili ya Tafsir ya Qur’an ni tafsir Bil Ray. Hii ni aina ya tafsir ya maneno au
        ibara au aya za Qur’an, kwa juhudi (ijtihad) ya kiakili (tafakuri), kwa kuangazia maana

        ya kiasili ya aya, lugha iliyotumika, na muktadha.

        Misingi ya tafsir Bil Ray


        Tafsir Bil Ray ni zao la juhudi (ijtihad), inayofanywa kupitia katika vyanzo vinavyokubalika
        kisheria. Misingi ya tafsir hii ni pamoja na:

            a)  Qur’an yenyewe na tafsir inayopatikana katika dhahiri yake;


            b)  Hadith za Mtume Muhammad (S.A.W) kuhusu jambo lililoelekezwa katika aya;

            c)  Athari za Maswahaba  zinazonasibiana na aya au ibara ya Qur’an inayokusudiwa
               kufafanuliwa;

            d)  Athari za Tabiin katika mwenendo wao wa maisha kulingana na aya husika;

            e)  Mazingira ya wakati uliopita, kipindi ambacho aya au sura husika imeteremshwa;
               na

            f)  Mazingira yaliyopo hivi sasa.




                                                 155
   160   161   162   163   164   165   166   167   168   169   170