Page 163 - EDK_F5
P. 163

SURA YA TANO                                                           KUFASIRI QUR’AN

        Ngazi za tafsir ya Qur’an

         Kazi ya 5 2

         Shirikiana na wanafunzi wenzako, kusoma matini kuhusu ngazi za tafsir ya Qur’an,
         kisha tofautisha baina ya tafsir Bil Maathur na Tafsir Bil Ray
        FOR ONLINE READING ONLY


        Kuna ngazi nyingi  za Tafsir ya Qur’an, tokea ilipotambuliwa kuwa ni fani ya elimu
        inayojitegemea karne ya tatu Hijriya hadi hivi sasa. Vimeandikwa vitabu vingi kuhusu
        sayansi ya Qur’an, kwa kuwa Qur’an yenyewe imesheheni taaluma mbambali ndani yake.
        Hata hivyo, kwa ujumla tafsir za Qur’an zinagawika katika ngazi mbili kubwa ambazo ni;
        Tafsir Bil Maathur na Tafsir Bil Ray.

        Tafsir Bil Maathur
        Hii ni ngazi ya kwanza ya tafsir ya Qur’an, ambayo inazingatia ufafanuzi wa baadhi ya
        aya za Qur’an kwa aya nyingine za Qur’an, ambazo zinabainisha zaidi kuhusu jambo
        lililoelezwa katika aya za awali. Kadhalika, tafsir Bil Maathur  inajumuisha ufafanuzi
        wa Qur’an uliotolewa na Mtume Muhammad (S.A.W), kisha ufafanuzi uliotolewa na
        maswahaba  zake,  kisha  ufafanuzi  uliotolewa  na  wanafunzi  wa Maswahaba  (Tabiin),
        kuhusu aya katika  Qur’an. Ni wazi  kuwa hakuna yeyote  anayeweza  kuifasiri  Qur’an
        kama Allah (S.W) mwenyewe, Mtume wake (S.A.W), Maswahaba (R.A) na wanafunzi
        wao (Tabi’in). Hivyo, ngazi hii ya tafsir inachukua daraja la kwanza.

        Miongoni mwa kazi mashuhuri za tafsir Bil Maathur ni pamoja na; Jaamiul Bayan Fiy
        Tafsirul Qur’an, iliyoandikwa na Imam Ibn Jarir Al-Twabari, aliyefariki mwaka 310H/
        923 M. Bahrul Ulumi iliyoandikwa na Abu Layth Nasr ibn Muhammad Al-Samarkand,
        aliyefariki mwaka 375 H. Al-Kashfu Wal-Bayan Tafsirul Qur’an, iliyoandikwa na Abu
        Is’haq Ahmad ibn  Tha’alab An-Naisaburi, aliyefariki  mwaka 427 H.  Tafsirul Qur’an
        Al-Adhwiim, iliyoandikwa na Imam Ismail ibn Amr ibn Kathir, aliyefariki mwaka 774H
        kama inavyoonekana katika kielelezo namba 5.3. Tafsir nyingine ni Ad-Durrul Manthur
        Fiy Tafsir Bil Maathur iliyoandikwa na mwanazuoni Jalaluddin Suyutwi. Hizi ni baadhi
        ingawa zipo nyingine, ambazo isingewezekana kuzitaja zote kwa sababu ya nafasi.


















                   Kielelezo namba 5.3: Juzuu za Tafsiri ya Qur’an ya Ibn Kathir.
                                                 153
   158   159   160   161   162   163   164   165   166   167   168