Page 166 - EDK_F5
P. 166

SURA YA TANO                                                           KUFASIRI QUR’AN

        Mitizamo  tofauti kuhusu tafsir Bil Ray
        Kuna maoni tofauti kuhusu aina hii ya tafsir, wapo wanazuoni wanaopinga njia hii ya

        tafsir, na wapo ambao wanaithibitisha. Wanaopinga njia hii wanatoa hoja kuwa, njia hiyo
        ya tafsir inaongeza maneno katika maneno ya Allah (S.W) bila mamlaka. Kwa kuwa
        hoja ya mfasiri wa rai itakuwa ni dhana pekee na hakuna uhakika kuwa hayo aliyosema
        FOR ONLINE READING ONLY
        ni makusudio halisi ya Allah (S.W). Kundi hili linaonesha kuhofia kutokana na Hadith
        ya Ibn Abbas, kuwa Mtume amesema; Yeyote yule atakayetoa maoni yake binafsi katika
        Qur’an ajiandalie makazi yake motoni.

        Wanazuoni wa Tafsir Bil Ray, wanakanusha hoja hiyo ya wanaopinga kwa kusema kuwa,
        ufafanuzi  unaotolewa  kwa kutegemea  ijtihad  stahiki,  unatoa maarifa  ya kutosha pale
        ambapo hakuna nusus ya wazi iliyoeleza jambo hilo.  Wanazuoni hao wanaifasiri Hadith

        ya Ibn Abbas kuwa ilimaanisha; kufafanua au kusema kitu katika Qur’an bila ya ushahidi
        au elimu au kwa utashi binafsi au ya kimadhehebu.

        Wanazuoni wa Tafsir Bil Ray wanatetea pia kukubalika kwa njia hii ya Tafsir, kwa kauli
        ya swahaba Abubakr (R.A), aliyesema kuwa; Nitatoa maoni yangu katika maneno ya
        Allah (S.W), kama nitapatia basi itakuwa ni kwa sababu ya mwongozo wake, lakini kama
        nitakosea basi ni makosa yangu mimi.


        Kwa  upande mwingine kukataza ijtihad katika kutafsiri Qur’an, kutafunga njia ya hukumu
        nyingi za kisharia katika changamoto nyingi na zinazozidi kujitokeza. Kwa ujumla, tafsir
        ya rai inayokatazwa ni ile inayofanywa kwa ujinga, uzushi na bila mazingatio.


        Ukiangaliwa mtazamo wa wanazuoni wanaopinga Tafsir Bil Ray na simulizi za baadhi
        ya Maswahaba na wanazuoni wakubwa wa kale, waliojiepusha  na kufasiri Qur’an,
        unagundua kwamba wote hao walijiepusha kwa sababu ya kiucha-Mungu, mashaka au
        wasiwasi na hofu ya kukosea kwa kuwa hapakuwa na hali zinazohitaji jambo hilo.

        Kwa hiyo, Tafsir Bil Ray zipo za aina mbili. Ya kwanza sio tu inakubalika bali inahitajika
        na kusisitizwa, wakati nyingine sio tu inatakiwa  kukatazwa  bali ni haram.  Tafsir Bil

        Ray, inayokubalika  ni ile  inayotimiza  vigezo, kama vile elimu  stahiki, kuepukana  na
        chembechembe za ujinga, hadaa na upotoshaji.

        Miongoni mwa Tafsir za rai mashuhuri na zinazokubalika ni pamoja na; Al-Tafsir al-Kabir
        (Mafatih Al-Ghayb) iliyoandikwa na Imam Fakhruddin Al-Razi kama inavyoonekana
        katika kielelezo  namba 5.4. Imam Fakhruddin  Al-Razi aliishi karne ya sita Hijriya
        (544 hadi 606H), Tafsir Al-Baydhwawi, iliyoandikwa na Kadhi Abdullah ibn ‘Umar Al-

        Baydhwawi, aliyeishi karne ya saba Hijriya na kufariki mwaka 691 H. Tafsir Jalalayn
                                                 156
   161   162   163   164   165   166   167   168   169   170   171