Page 42 - EDK_F5
P. 42

SURA YA KWANZA                                                   ELIMU KATIKA UISLAMU

        hii ni jambo la kihistoria  lenye kudumu ambalo  pia limempatia  mwandishi, heshima
        na umaarufu duniani. Humo kuna kumbukumbu ya mambo ya kihistoria, juu ya aina
        mbalimbali za ustaarabu duniani uliotokana na athari za mazingira na hali ya hewa tofauti,

        maisha ya makazi ya kibedui (ya kuhamahama) na ya kudumu pamoja na tamaduni tofauti
        tofauti za jamii hizo na pia taasisi tofauti za kijamii, sayansi na sanaa zao. Mwandishi pia
        FOR ONLINE READING ONLY
        anaongelea masuala ya sayansi, hesabu, muziki na ala zake, kilimo na sanaa kwa mujibu
        wa Qur’an. Kwa kweli, ni kazi yenye maelezo kuhusu mambo mengi na yaliyoelezwa
        kifasaha ambapo historia yenyewe imeelezewa kuwa ni sehemu ya somo la Falsafa kwa
        maneno yafuatayo: “Hebu tutazame undani wa somo la Historia”, anasema Ibn Khaldun
        kwamba, ni uchunguzi na uthibitisho wa taarifa, uchunguzi makini wa sababu za kuwepo

        kwa mambo (kama yalivyo) na uelevu wa kina wa jinsi mambo yalivyoweza kutokea.
        Hivyo, Historia ni mojawapo ya sehemu za somo la Falsafa, na inapaswa kutambuliwa
        kama mojawapo ya elimu ya sayansi.” Hii kwa kweli ndiyo dhana ya kileo juu ya somo
        la Historia, kutokana na kuuona umuhimu na nafasi yake katika uchambuzi wa taarifa
        mbalimbali na kutafuta chanzo au sababu za mambo. Historia inapaswa kuwa ni elimu ya
        kudumu katika ustaarabu wa mwanadamu na saikolojia yake.


        Ni vigumu kuweza kuchambua kwa kina kazi kubwa aliyoifanya Ibn Khaldun.Uchunguzi
        wake adilifu juu ya upoteaji na uharibifu wa staarabu mbalimbali, katika mzunguko, na
        mchango mkuu wa wasomi katika uundaji wa mataifa mbalimbali, ambao amewanukuu
        katika jitihada za kuhami dhana yake, ni mambo yenye kuvutia. Ibn Khaldun alibobea pale
        alipoainisha maisha ya taifa lolote na ya watu au ya kiumbe kingine chochote, kwamba
        hata mataifa yanazaliwa, yanakua na yanakufa. Pia, kwamba mataifa yako chini ya kanuni
        ya mabadiliko asilia. Ibn Khaldun amehusika na uvumbuzi wa kanuni hii ya mabadiliko
        ya taifa lolote.


        Uchumi

        Ibn Khaldun, mawazo yake ya kiuchumi kama ya kisiasa, yameendelea kutumika hata
        leo. Mwandishi huyu kutoka iliyokuwa ikiitwa Maghreb (Morocco) anasema: “Taifa ni
        sawa na mfanyabiashara mkubwa, kwani ana jukumu la kuhakikisha kuwa pesa azipatazo

        kutokana na kodi, zinarudi na kuwazungukia watu. Kodi za wastani ni motisha tosha ili
        watu waweze kujituma katika kufanya kazi. Kwa upande mwingine, kupandisha kodi
        yoyote tena kiholela holela, kunaweza kusababisha yasipatikane mafanikio ya malengo
        ya kodi husika.” Anachunguza kwa makini sana masuala ya utaifishaji au ushikiliaji wa
        mali za watu, ukiritimba, usimamizi na udhibiti wa biashara kabla ya kuhitimisha kwa
        kusema kwamba rasilimali za taifa, misingi yake mikuu ni watu, ari ya makampuni yake


                                                  32
   37   38   39   40   41   42   43   44   45   46   47