Page 43 - EDK_F5
P. 43

SURA YA KWANZA                                                   ELIMU KATIKA UISLAMU


        ya kibiashara na tija katika ufanyaji wa shughuli zote za kiuchumi.

        Kujiingiza  kwa  serikali  katika  utendaji  wa shughuli  za  kiuchumi  hupunguza  uwezo
        wa uzalishaji na utumiaji wa rasilimali za Taifa na hivyo huchelewesha upatikanaji wa

        maendeleo katika jamii. Ukweli ni kwamba, taaluma ya siku hizi katika dhana ya uchumi
        FOR ONLINE READING ONLY
        huria haikuongeza lolote katika mtizamo kama huu, ambao ulishajengeka tangu karne ya
        15.


        Sehemu kubwa ya elimu hizi ilikuwa imehifadhiwa katika maktaba mbalimbali za umma
        na binafsi. Palikuwa na vitabu vingi mno ukilinganisha na zama zenyewe; kwa mfano
        Darul Hikma huko Cairo (karne 11) ilikuwa na vitabu milioni 1.6, Baitul Hikma, Baghdad
        (karne ya 8) palikuwa na vitabu vingi sana, wakati maktaba ya Al-Hakm, Hispania ilikuwa

        na vitabu laki 4 na ile ya Bani Ammar Tripoli ilikuwa na vitabu milioni moja.

        Waislamu walipoanza kusahau jukumu lao la ukhalifa, na wakashughulishwa zaidi na
        mambo  ya anasa na wengine kuanza  kuyaendea  maisha  ya kitawa,  maadui  walianza

        kuichukua nafasi hiyo kidogo kidogo. Mgawanyo wa elimu nao ulipochukua nafasi yake,
        Waislamu  walianza  kuwa duni na mara  kuvamiwa  na maadui  zao. Wamongolia,  kwa
        mfano, walivamia Baghdad na kuvitupa vitabu vingi sana katika mto Trigis, hadi mto huo
        kufurika na maji kugeuka rangi nyeusi, kwa sababu ya wino. Huko Hispania, ilipotekwa

        Dola ya Kiislamu na Wakristo, vitabu milioni moja vilikuwa vikichomwa moto kila siku!
        Vitabu vingine vilivyoandikwa na Waislamu vilitafsiriwa kwa lugha nyingine; Kifaransa,
        Kilatini, Kiitaliana n.k hivyo Wazungu wakatumia nafasi hiyo kujidai uandishi.


        Kilimo na viwanda

        Katika fani ya kilimo na viwanda, aidha wanazuoni Waislamu walikuwa ndio viongozi. Ibn
        Awwami aliweza kuainisha aina 585 za mimea, na kuitolea maelezo ya namna ya kuikuza.

        Abu-Abbas An-Nabati (Abu Abbas, the Botanist yaani Abu Abbas, bingwa wa elimu ya
        mimea), alikuwa akizunguka bahari ya Sham hadi Afrika, kukusanya aina mbalimbali
        za mimea. Kwenye nchi ya Syria, kulikuwa na viwanda vya ufumaji, kutengeneza kauri,
        nguo za pamba, ngozi, madini, glasi na vyuma. Elimu ya Kemia, ilitumika kutengeneza

        marashi  na mafuta  mazuri  kutoka  kwenye maua  ya waridi.  Utengenezaji  wa karatasi
        ulikuwa umeshitadi kila upande, kwa kuwa huwezi kuhimiza kusoma bila ya kuwa na
        zana za kuandikia.




                                                  33
   38   39   40   41   42   43   44   45   46   47   48