Page 44 - EDK_F5
P. 44

SURA YA KWANZA                                                   ELIMU KATIKA UISLAMU



          Ufupisho


          Uislamu unaitazama elimu kuwa ni ujuzi ulioambatanishwa na utendaji. Aliyeelimika ni
          yule aliyebadilika tabia na mwenendo wake kutoka katika hali duni kiutendaji, kuelekea
        FOR ONLINE READING ONLY
          hali ya ufanisi kutokana na ujuzi alioupata darasani au nje ya darasa, vitabuni au katika
          mazingira yaliyomzunguka. Aliyesoma bila kutafsiri alichokisoma katika matendo ya
          kila siku ni sawa tu na asiyesoma kwa sababu wote hawa hawainufaishi jamii.

          Malengo  ya  elimu  katika  Uislamu  ni  kumuwezesha  mja  kumtambua Allah  (S.W),
          kuliendea na kulifikia lengo la kuumbwa kwake ambalo ni kumuabudu Allah (S.W).
          Mja hawezi kumuabudu Allah (S.W) mpaka awe Khalifa. Yaani aweze kuiongoza jamii
          kwa kufuata mwongozo wa Allah (S.W). Mfumo wa elimu wa Kiislamu ndio wenye
          kumuwezesha mwanadamu kufikia malengo haya na kuikomboa jamii katika dimbwi
          la ujinga na ujahili.

          Elimu ya Kiislamu ni elimu inayojihusisha na fani zote za elimu, zinazosomwa kwa
          kuzingatia  lengo  la  elimu  kwa  mujibu  wa  Uislamu  na  kumtafakari  Allah  (S.W).
          Mwalimu wa fani ya Qur’an,  Tarekh, Fiqh,  Akhlaq,  Kemia, Biolojia  na Fizikia,
          anakuwa  anafundisha  elimu  ya  Kiislamu  madhali  anazingatia  tafakuri  juu  ya Allah
          (S.W).


          Mgawanyo wa elimu ya dini na elimu ya dunia kama unavyopigiwa zumari na makafiri
          na baadhi ya Waislamu, wasiojua makusudio halisi ya mgawanyo huo, haukubaliki
          katika Uislamu. Mgawanyo huo husababisha Waislamu kutoipa kipaumbele elimu ya
          mazingira, Wasomi Waislamu kutoipa thamani stahiki dini yao na Waislamu kushindwa
          kuwa Makhalifa wa Allah (S.W) katika jamii.

          Kwa kuwa kutafuta elimu ni faradhi kwa kila Muislamu, zama zote Waislamu wamekuwa
          wakifanya juhudi za makusudi katika  elimu,  jambo ambalo  limewafanya  kubobea
          na kugundua fani mbalimbali za elimu ikiwa ni pamoja na tiba, fizikia, unajimu na
          kadhalika. Waislamu waliharibikiwa na kuwa duni kama hivi sasa pale walipokumbwa
          na fitina ya Makafiri ya kutenganisha maisha ya dini na maisha ya dunia yaliyoambatana
          na mgawanyo wa elimu katika tapo la dini na dunia.

          Waislamu wanaweza kurudi katika hadhi yao ya juu katika jamii, endapo kila Muislamu
          atajizatiti kusoma elimu ya mwongozo na mazingira kwa lengo la kumuabudu Allah
          (S.W) katika kila kipengele cha maisha yake ya kibinafsi na kijamii na kwa lengo la
          kusimamisha Ukhalifa katika jamii.




                                                  34
   39   40   41   42   43   44   45   46   47   48   49