Page 49 - EDK_F5
P. 49

SURA YA PILI                                                    ITIKADI KATIKA UISLAMU


        wa mifumo inayoundwa na mwanadamu. Hivyo, katika sehemu hii, zimeangaziwa tofauti
        za itikadi katika sehemu kuu mbili:
        a) Itikadi na madhara ya dini zilizobuniwa na wanadamu
        b) Ubora wa Itikadi na usahihi wa dini ya Uislamu
        FOR ONLINE READING ONLY
        Itikadi ya Ukafiri

        Ukafiri ni dini iliyojengwa kwa misingi ya kukana kuwepo kwa Allah (S.W), Muumba wa

        viumbe vyote. Ukafiri unaitakidi mambo yafuatayo:
          i.   Hakuna Mungu Muumba wa vitu vyote ulimwenguni.  Lakini  viumbe vyote
               vimetokea kwa bahati nasibu;

         ii.   Hakuna malengo na makusudio maalumu ya kuumbwa viumbe, hivyo mwanadamu
               hana lengo ila kuishi tu. Kwa maana lengo la kuishi mwanadamu hapa duniani ni

               kupata mahitaji ya maisha na kuendeleza maisha;

         iii.   Kwa kuwa hakuna Mungu Muumba wa ulimwengu, mwanadamu kwa ujuzi wake
               alionao, ana jukumu la kujiundia mfumo wa maisha wenye manufaa kwake, ili
               kuishi kwa amani na furaha hapa duniani; na

         iv.   Kwa kuwa mwanadamu na maumbile yote vimetokea kwa bahati nasibu, hivyo

               mwisho wa maumbile yote ni kutoweka kwa bahati nasibu. Kwa maana nyingine
               makafiri  wanaitakidi  kuwa  hapana  maisha  mengine  baada  ya  maisha  ya  hapa
               duniani.
        Itikadi hii imebainishwa bayana katika Qur’an, pale Allah (S.W) anaposema:
                                               َ
                                                          ۡ
                          ۡ
                                  َ
                                                                  َ
                  ُ  َ  َ َ ُ َّ  َّ ٓ ُ  ۡ ُ َ َ َ ۡ َ ُ ُ  َ  َ ُّ  َ ُ َ  َّ  َ  َ  ْ ُ َ  َ
                 مهل امو ۚرهلدٱ لِإ انكِلهي امو اينو تومن اينلدٱ انتايح لِإ  ِ ه ام اولاقو
                                                     َ ُّ ُ َ  َّ  ۡ ُ ۡ  ۡ  ۡ  َ َ
                                                                                 ٰ
                                                  ٢٤نونظي لِإ مه نِإ ملِع نِم كِلذب
                                                                      ٍۖ
                                                                                   ِ
                Na walisema: “Haukuwa (uhai) ila ni uhai wetu huu wa dunia,(hakuna
                mwingine);  tunakufa  na tunaishi,  wala  hakuna  kinachotuangamiza
                isipokuwa  (huu  huu)  ulimwengu;  (kwani  ndiyo  ada  yake  kufisha  na
                kuhuisha).” Lakini  wao hawana ilimu  ya  hayo  (wanayoyasema)
                wanadhani tu.” (Al-Jathiyah, 45: 24)

        Madhara ya itikadi ya Ukafiri

        Itikadi ya Ukafiri ina madhara katika jamii, yanayoweza kujumuishwa katika vipengele
        vifuatavyo:


                                                  39
   44   45   46   47   48   49   50   51   52   53   54