Page 47 - EDK_F5
P. 47

SURA YA PILI                                                    ITIKADI KATIKA UISLAMU

         Maswali:


         1. Aya hii inazungumzia kitu gani?

         2. Unapata mafunzo gani kutokana na aya hii?
        FOR ONLINE READING ONLY
        Maana ya itikadi


        Wataalamu wametoa maana mbalimbali za itikadi kwa mujibu wa mitazamo yao. Katika
        uwanja  wa sosiolojia,  itikadi  inarejelewa  kama  jumla  ya  maadili,  imani,  mawazo  na
        matarajio  ya mtu. Itikadi  ipo ndani ya jamii,  makundi, na baina ya watu. Hubuniwa
        mawazo, matendo, na utangamano wa watu, pamoja na kile kinachotokea katika jamii
        kwa ujumla.

        Ama kwa upande wa wanazuoni wa Kiislamu, itikadi wanaifasiri kuwa ni msimamo wa
        mtu juu ya maarifa ya kitu fulani, unaofungamana moyoni kupitia imani, sawa uwe sahihi
        au wenye makosa. Kwa mujibu wa wanazuoni wa Kiislamu, itikadi imejikita zaidi katika
        masuala yanayofungamana na dini. Kwa muktadha huo, itikadi inajikita juu ya fikra na
        imani za kidini sawa dini hiyo iwe sahihi au isiwe sahihi.

        Aina za itikadi

         Kazi ya 2 2


         Shirikiana na wanafunzi wenzako kuchunguza kielelezo namba 2.1 na kutoa tafsiri ya
         alama zilizomo katika kielelezo hicho





        Kuna aina kuu mbili za itikadi: itikadi za wanadamu na itikadi ya Mola Mlezi. Katika
        kundi la itikadi  za wanadamu  zilizo  maarufu  zaidi  ni itikadi  za kisiasa, na itikadi  za
        kiepistemolojia. Epistemolojia ni sehemu ya falsafa inayohusu utafiti wa jinsi mambo
        yanavyojulikana.


        Itikadi  ya kisiasa, hujikita  katika  upangiliaji  wa mawazo ya kimaadili  na vipi nchi
        iendeshwe.Wakati, itikadi za kiepistemolojia hujihusisha na upangiliaji wa mawazo ya
        kifalsafa, ulimwengu, na jinsi gani watu wanapaswa kufanya maamuzi. Kwa muktadha
        huo, katika  itikadi  za  wanadamu,  kunapatikana  aina  nyingine  ndogondogo za  itikadi.
        Moja kati ya hizo ni pamoja na Ukomunisti, Usoshalisti na Ubepari; itikadi hizo hujikita
        katika nyanja za kiuchumi na kisiasa kwa ujumla. Kwa kuwa itikadi zote zinahusisha
        mwanadamu na maisha yake, mwanadamu huchagua aina moja au zaidi katika kuendesha

                                                  37
   42   43   44   45   46   47   48   49   50   51   52