Page 48 - EDK_F5
P. 48

SURA YA PILI                                                    ITIKADI KATIKA UISLAMU
        maisha yake. Hivyo, itikadi inafungamana na mfumo wa maisha, ambao ndio dini. Dini
        zenyewe zimegawika katika makundi makubwa mawili:

         (i)  Dini ya Allah (S.W) inayojulikana kwa jina la Uislamu, na
         (ii) Dini zilizoundwa na wanadamu, ambazo nazo zimegawika katika makundi makuu
             matatu yafuatayo:
        FOR ONLINE READING ONLY
            a) Dini ya Ukafiri
            b) Dini ya Ushirikina
            c) Dini ya Utawa












































                                Kielelezo namba 2.1: Nembo za Itikadi.
        Tofauti za itikadi na athari zake


        Itikadi za dini zilizobuniwa na wanadamu zina madhara mbalimbali, kwa kuwa zimebuniwa
        na kiumbe mwenye udhaifu, katika milango anayoitumia kutafakari na kutolea maamuzi;
        macho,  masikio,  ngozi,  ulimi,  na akili.  Ukiachana  na udhaifu  huo, pia  mwanadamu
        ametawaliwa na matamanio ya nafsi, hivyo chochote anachokibuni huwa kwa lengo la
        maslahi yake binafsi. Hana tabia ya kuwanufaisha wengine. Hii nayo ni sababu ya udhaifu


                                                  38
   43   44   45   46   47   48   49   50   51   52   53