Page 45 - EDK_F5
P. 45

SURA YA KWANZA                                                   ELIMU KATIKA UISLAMU


         Zoezi la marudio la 1

         1.  Fafanua faida za kusoma kwa kuzingatia malengo ya elimu katika Uislamu


         2.  Mifumo  ya elimu inayotokana na  mifumo ya maisha iliyobuniwa na wanadamu
        FOR ONLINE READING ONLY
             ina changamoto. Fafanua kauli hiyo kwa kurejea mfumo wa elimu wa Ujamaa na
             Ubepari

         3.  Kwa mujibu wa Uislamu, eleza madhara matano ya kuitumia elimu nje ya lengo
             lake

         4.  Chambua sifa tatu zinazobainisha elimu yenye manufaa katika jamii

         5.  Fafanua madhara matano ya mgawanyo wa elimu ya dini na elimu ya dunia katika
             jamii inayokuzunguka

         6.  Baadhi ya watu katika jamii wanadai kwamba chimbuko la fani za elimu zilizopo
             duniani zimetokana na mwanadamu mwenyewe. Thibitisha au kanusha madai hayo
             kwa kutumia hoja tano


         7.  Bainisha mchango wa Waislamu katika maendeleo ya sayansi na teknolojia kwa
             kuzingatia fani zifuatazo:

             (a)  Unajimu

             (b)  Jiografia


             (c)  Hisabati

             (d)   Kemia

             (e)  Elimu ya Tiba






















                                                  35
   40   41   42   43   44   45   46   47   48   49   50