Page 176 - Fasihi_Kisw_F5
P. 176

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




              Uhariri:           Kazi ya kusoma, kusahihisha na kusanifu miswada kama vile
                                 makala au vitabu

              Uigizaji:          Tendo la kuchukua vitu kutoka nje na kuviingiza  ndani ya
                                 sehemu au eneo lenu jukwaa
          FOR ONLINE READING ONLY
              Ujumi:             tathmini inayobainisha ubora au ubaya wa kazi za kisanaa
              Ujuzi:             Ufundi au utaalamu  au maarifa  alionayo  mtu  katika  kufanya
                                 shughuli fulani
              Uketo/ utao:         Kipande cha pili katika mshororo

              Ukwapi:            Kipande cha kwanza katika mshororo
              Umahiri:           Ni ujuzi mkubwa wa kufanya jambo fulani

              Upeo:              Ni mstari wa mwisho katika ubeti wa shairi
              Usawiri:           kutoa sura halisi ya kitu

              Ushairi:           Utanzu wa fasihi ambao hutumia sauti zilizopangiliwa, mizani,
                                 lugha  ya  mkato,  lugha  ya  mafumbo  na  uimbaji  au  ughani  ili
                                 kuwasilisha kwa hadhira maudhui yaliyokusudiwa
              Utafiti:             Uchunguzi wa kitaalamu  wa jambo kwa kukusanya data na
                                 kuzichambua ili kupata ukweli wa jambo fulani
              Utamaduni:         Mfumo wa maisha wa jamii  fulani  unaojumuisha  mila,  jadi,
                                 desturi na sanaa za kundi la jamii fulani
              Utanzu:            Kundi linalojumuisha kazi mbalimbali za sanaa zenye kuchangia
                                 sifa fulani kuu
              Utendi:            Utungo mrefu wa kishairi unaozungumzia kwa mapana matendo
                                 ya kihistoria ya shujaa
              Utenzi:            Utungo mrefu wa kishairi unaohusu mawaidha au masuala
                                 mengine ya kijamii
              Utomeleaji:        uchopekaji  wa kipengele  cha  kipera  fulani  kwenye  utanzu
                                 tofauti. Mfano kipera cha nyimbo kikitumika kwenye riwaya au
                                 hadithi fupi

              Utunzi:            Utungaji wa kazi yoyote ya kifasihi
              Wimbo:             Utungo wa kimuziki  unaowasilishwa kwa kuimbwa  na
                                 huzingatia mahadhi maalum
              Zana:              Kitu ambacho mtu hukitumia kufanyia shughuli fulani









                     Kitabu cha Mwanafunzi                                           165
                        Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   165                   23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   165
   171   172   173   174   175   176   177   178   179   180   181