Page 174 - Fasihi_Kisw_F5
P. 174

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




              Nahau:             Misemo  ya  picha  ambayo  huwa  na  maana  iliyofichika.  Kwa
                                 kawaida, huundwa na kitenzi na nomino

              Nathari:           Utungo unaotumia lugha ya mjazo
              Ngano:             Hadithi za kimapokeo  zitumiazo  wahusika kama wanyama,
          FOR ONLINE READING ONLY
                                 miti na watu kuelezea na kuonya kuhusu maisha. Maudhui yake
                                 hujikita katika maadili, mahusiano na mwenendo ndani ya jamii

              Ngoma:             Kipera cha sanaa za maonesho za jadi  ambacho  huhusisha
                                 uchezeshaji wa viungo vya mwili wenye mtindo na miondoko
                                 maalumu  inayoambatana  na muziki.  Pia ni kifaa  cha muziki
                                 kilichowambwa kwa ngozi

              Ngomezi:           Fasihi itumiayo midundo ya ngoma ili kuwasilisha ujumbe
              Ngonjera:          Mazungumzo au majibizano ya kishairi ya kusemwa yanayohusu
                                 mada fulani
              Programu:          Mfumo wa kompyuta ulioandaliwa kwa ajili ya kutenda kazi
                                 fulani  kama  vile  kutengeza  vitabu,  kupeleka  au  kupokea
                                 baruapepe

              Ramsa:             Aina ya tamthiliya inayokusudia kufurahisha au kuchekesha, na
                                 huwa na mwisho mwema

              Riwaya:            Hadithi ndefu ya kubuni itumiayo lugha ya kinathari (lugha ya
                                 mjazo) na yenye uchangamani wa visa, wahusika, mandhari na
                                 dhamira
              Sanaa:             Ufundi wa kuwasilisha  hisia  na mawazo  ya binadamu  kwa
                                 maandishi, michoro, uchongaji, ufumaji na kadhalika
              Sanifu:            Weka taratibu za lugha zenye kufuata kanuni zinazokubalika

              Shairi:            Utungo  wenye  mishororo  au  mistari  iliyogawanywa  kwenye
                                 mafungu  kadhaa  unaoeleza au  kuonesha  kwa ufupi  wazo  au
                                 jambo au hisia fulani kuhusu binadamu na mazingira yake kwa
                                 lugha ya picha na mkato

              Sitiari:           Tamathali ya usemi inayotumika kuonesha ulinganishi wa vitu
                                 au hali tofauti bila ya kutumia maneno ya ulinganishi

              Soga:              Hadithi fupifupi za utani na ucheshi
              Sokrate:           Mwanafalsafa wa Kiyunani aliyeishi 469 - 399 K.K

              Taashira:            Tamathali ya usemi ambapo jina la sehemu ya kitu hutumika
                                 kuwakilisha kitu kamili

              Tabaini:           Tamathali za semi inayosisitiza jambo kwa kutumia maneno au
                                 kauli kinzani





                     Kitabu cha Mwanafunzi                                           163
                        Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   163                   23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   163
   169   170   171   172   173   174   175   176   177   178   179