Page 169 - Fasihi_Kisw_F5
P. 169

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




              (g)  Taharuki
              Hadithi  za  watoto  hutumia  taharuki  ili  kumtamanisha  mtoto  kufahamu  tukio
              linalofuata, kujua zaidi kuhusu matokeo ya mgogoro unaoendelea na kumfanya
              adadisi  zaidi  kuhusu mtiririko  wa hadithi  hiyo.  Mfano  mzuri  wa uundaji  wa
          FOR ONLINE READING ONLY
              taharuki ni pale mhusika anapokuwa katika tukio la hatari ambalo mtoto hajui
              hatima yake. Kwa hiyo, hutamani kusoma zaidi ili ajue mustakabali wake.

              (h)  Fantasia
              Hadithi za watoto hutumia matukio, matendo na vitu visivyo vya kawaida, dhana
              halisi na zile zenye maajabu ili kujenga taharuki na kuibua dhamira mbalimbali.
              Mfano wa hadithi hizi ni pamoja na Marimba ya Majaliwa (Semzaba, 2008)

              (i)  Usimulizi
              Usimulizi ni uwasilishaji wa kimfuatano wa matukio katika kazi ya fasihi kama
              vile mashairi, tamthiliya,  riwaya, hadithi fupi. Katika kazi nyingi za fasihi,
              usimulizi wake ni wa nafsi ya kwanza au ya tatu. Vilevile, upo usimuliaji wa
              nafsi ya pili. Katika tamthiliya, usimulzi hujitokeza katika mchanganyiko wa
              maelekezo ya jukwaa na mazungumzo baina ya wahusika au hata mandhari au
              muonekano wa wahusika.

              (j)  Dhamira zenye mafunzo chanya
              Hadithi za watoto hupaswa kuwa na maudhui ya kuburudisha na yenye mafunzo
              yanayowafaa. Kama ilivyo kawaida, dhamira huwa hazibainishwi wazi bali
              msomaji  hujenga maana  kutokana  na kile kinachosimuliwa. Hivyo, mtoto
              anatakiwa kujengewa dhamira rahisi na kadri anavyokua ajengewe dhamira za
              kufikirisha. Dhamira za watoto huweza kujengwa kwa kumfanya mtoto kutambua
              vitu na mazingira, urafiki, mahusiano ya kifamilia, makuzi bora na kukabiliana
              na hali tofauti za maisha.

               Shughuli ya 6.12

              Chagua mada moja kati ya zifuatazo, kisha tunga hadithi ya watoto kulingana
              umri utakaochagua.


              Mada za uandishi
                   (i)  Safari ya ajabu

                   (ii)  Maisha ya shule
                   (iii)  Msitu wa ajabu

                   (iv)  Watoto wa mtaani
                   (v)  Mwanga wa elimu


               158                                                 Kitabu cha Mwanafunzi
                                                                     Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   158
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   158                   23/06/2024   17:54
   164   165   166   167   168   169   170   171   172   173   174