Page 168 - Fasihi_Kisw_F5
P. 168

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




              na  umri  wao.  Urahisi  huo  hutokana  na  sentensi  kuwa  fupi  na  uteuzi  wa
              msamiati unaoendana na kiwango chao. Vilevile, inashauriwa mwandishi wa
              hadithi arudierudie maneno, sentensi na vifungu vya maneno ili kumsaidia
              mtoto kuelewa suala linalowasilishwa. Hata hivyo, lugha inayotumika huweza
          FOR ONLINE READING ONLY
              kutofautiana kutokana na rika, umri na ngazi ya usomaji, kama vile ngazi ya
              awali, shule za msingi na vijalunga chini ya miaka 18.

              (b)  Wahusika
              Mara nyingi, wahusika ni watoto au wale wanaoakisi matendo ya rika lengwa,
              yaani  watendao  au  kuzungumza  kitoto.  Majina  ya  wahusika  yasifanane  wala
              yasikaribiane ili kutokuwachanganya watoto. Kwa mfano si vizuri kwenye kazi
              moja kutumia majina kama Avita na Avera, Paula na Paulo; Samiri, Samira na
              Samri; au Petro, Petronia, na Petrobasi. Vilevile, ni vyema mhusika abainishwe
              wazi kwa kuzingatia umbo, sifa, rangi, mavazi na tabia zake.

              (c)  Msuko wa visa na matukio
              Hadithi za watoto hujengwa kwa msuko rahisi na wa moja kwa moja ambapo
              kisa huwa na chanzo, kati na mwisho. Kwa mfano, mhusika anatambulishwa
              akiwa anazaliwa, anasoma shule, mwisho anapata kazi. Vilevile, matukio yawe
              na taharuki ili kuwavutia watoto kutamani kuendelea kusoma hadithi.

              (d)  Picha na michoro
              Hadithi  za  watoto  huwa na picha  na michoro  mingi  kwa ajili  ya kufafanua
              zaidi maelezo, kuibua hisia, kurahisisha uelewa wa tukio linalowasilishwa,
              kujenga kumbukumbu, kuongeza ubunifu na kuvutia watoto. Picha hizo huweza
              kupambwa kwa rangi mbalimbali kutegemeana na maudhui na rika husika.


              (e)  Mandhari halisi
              Mara nyingi, hadithi za watoto zinapaswa kusawiri miktadha  ya kijamii
              au  kitamaduni  inayowafaa  watoto.  Vilevile,  mandhari  za  hadithi  za  watoto
              zibainishwe  wazi, zisiwe za kuwakatisha  watoto tamaa  ya kusoma suala
              linaloweza  kuwafanya washindwe kuendelea  kuisoma hadithi. Inashauriwa
              katika hadithi za watoto wadogo, rika la awali na kati, zitumike mandhari halisi.

              (f)  Taswira
              Hadithi za watoto ziwe zinafikirisha na kuwajengea hisia na picha mbalimbali
              akilini  mwao ili  kuwachangamsha.  Taswira hujengwa kwa kutumia  lugha  ya
              picha, tamathali za semi na mbinu nyingine za kisanaa zinazohusiana na umri
              wao.




                     Kitabu cha Mwanafunzi                                           157
                        Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   157                   23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   157
   163   164   165   166   167   168   169   170   171   172   173