Page 163 - Fasihi_Kisw_F5
P. 163

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




              (j)  Kuboresha
              Baada ya rasimu ya kwanza kukamilika, mtunzi anatakiwa kupitia au kukagua
              kazi yake ili kufanya maboresho ya kiutungaji na kiubunifu. Mwandishi anaweza
              kurekebisha mpangilio wa visa na matukio na kuongeza au kupunguza mambo
          FOR ONLINE READING ONLY
              yanayojirudia na yasiyokuwa na maana, au hata kubadilisha muundo wa sehemu
              kadhaa  za  kazi  yake.  Vilevile,  mtunzi  anaweza  kuwasuka upya wahusika ili
              kuendana na mwelekeo wa usimulizi na matumizi ya lugha ili kuifanya kazi ivutie
              na kuwa na kipekee. Pia, katika mchakato huu mwandishi anaweza kuboresha
              miundo ya sentensi kwa kuondoa maelezo yasiyo ya lazima ili kuweka urahisi wa
              kueleweka kwa wasomaji. Kwa hiyo, ni muhimu mwandishi kupitia kazi yake
              mara baada ya uandishi ili kuhakikisha kazi ina mtiririko wenye mantiki, usahihi
              wa taarifa, ushikamani wa kiusimulizi na ufikishaji wa ujumbe uliokusudiwa.


              (k)  Kuhariri
              Hii ni hatua muhimu katika mchakato wa uandishi wa kazi za kifasihi. Katika hatua
              hii, mwandishi anang’arisha na kuboresha maandishi ya kazi yake ili kuifanya
              iwe sahihi na inayoeleweka kwa wasomaji. Hivyo, mtunzi hupaswa kuhariri kazi
              yake kwa kuondoa makosa ya kiuandishi, kiuakifishaji na kimsamiati kama vile
              sarufi, miundo ya sentensi na matumizi sahihi ya maneno. Vilevile, mwandishi
              huweza kuhariri kazi yake kwa kuweka mtiririko  mzuri wa uwasilishaji  wa
              matukio, mawazo na hisia ili kuifanya kazi ivutie zaidi. Mtunzi yupo huru kumpa
              mtu mwingine ili ahariri kazi yake, hususani mtaalamu  aliyebobea  kwenye
              utanzu husika na baadaye mhariri wa lugha. Hata hivyo, ingawa mchakato huu
              ni muhimu ni vyema kuhakikisha kuwa uhariri hauharibu ubunifu na mtindo wa
              lugha wa mwandishi.

              (l)  Kupitia kwa mara mwisho
              Hii ni hatua ya mwisho katika uandishi, ambapo mwandishi huisoma upya kazi
              yake ili kuchunguza na kurekebisha makosa madogomadogo kama vile tahajia
              na sarufi. Lengo la usomaji huu ni kuhakikisha kazi inazingatia ubora, usahihi na
              ufasaha. Baada ya hatua hii, kazi itakuwa imekamilika. Hivyo, inaweza kuendelea
              na hatua za uchapishaji kutegemeana na malengo ya mwandishi.

               Shughuli ya 6.6
              Kwa kutumia vyanzo vya mtandaoni, maktabani au vinginevyo, jadili umuhimu
              wa kufuata hatua za uandishi wa kazi ya fasihi.









               152                                                 Kitabu cha Mwanafunzi
                                                                     Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   152
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   152                   23/06/2024   17:54
   158   159   160   161   162   163   164   165   166   167   168