Page 160 - Fasihi_Kisw_F5
P. 160
Fasihi ya Kiswahili kwa Shule za Sekondari
Zoezi la 6.2
1. Jadili hoja kwamba matumizi ya TEHAMA yana athari katika kazi za
FOR ONLINE READING ONLY
fasihi ya Kiswahili.
2. Jadili umuhimu wa kutumia majukwaa ya kidijiti katika kusambaza kazi
za fasihi ya Kiswahili.
3. Kwa kutumia mifano, fafanua namna uigizaji unavyoweza kuwa fursa
ya kukuza uchumi.
4. “TEHAMA haina mchango wowote katika kuchangia miktadha ya
utunzi wa kazi za fasihi”. Jadili.
Shughuli ya 6.5
Kwa kutumia vyanzo vya mtandaoni na maktabani, jadili hatua za utunzi wa kazi
za kifasihi.
Hatua za utunzi wa kazi za fasihi
Uandishi wa kazi za fasihi huongozwa na hatua mbalimbali ambazo hutegemeana
na kukamilishana. Mtunzi wa maigizo, mashairi au hadithi za watoto hana
budi kuzingatia hatua hizo ili aweze kuandika kazi yenye ubora na ushawishi.
Uandishi wa kazi za fasihi unaweza kujumuishwa katika hatua kuu tano ambazo
ni: maandalizi, uandishi/utungaji, uboreshaji, uhariri, na mapitio ya mwisho.
Ufuatao ni ufafanuzi wa hatua hizi:
(a) Kufanya maandalizi
Katika hatua ya maandalizi, mwandishi anaweza kujiuliza maswali kadhaa
kuhusu uandishi wake. Mifano ya maswali hayo ni: Ni jambo gani anataka
kuandika? Kwa nini aandike kuhusu jambo hilo? Anamwandikia nani? Wapi
atapata ukweli/uhakika kuhusu mambo anayotaka kuandika? Vifaa gani muhimu
vinahitajika katika uandishi wake? Maswali haya yanadokeza mambo muhimu
ambayo mwandishi anapaswa kuyafanya kabla ya mchakato mzima wa uandishi.
Hivyo, katika hatua hii, mtunzi hupaswa kubuni wazo au mada ya uandishi, na
kuanza kufanya uchunguzi kuhusu mada hiyo, na kuamua kuhusu utanzu wa
Kitabu cha Mwanafunzi 149
Kidato cha Tano
23/06/2024 17:54
FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd 149 23/06/2024 17:54
FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd 149