Page 157 - Fasihi_Kisw_F5
P. 157

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




              fasihi husaidia kueneza utamaduni na sanaa ya jamii husika. Hivyo, kazi za fasihi
              huweza kutoa fursa mbalimbali ambazo huinua pato la mtu binafsi na taifa kwa
              ujumla. Ufuatao ni baadhi ya ufafanuzi wa fursa hizo:


              Fursa mojawapo  ya  kazi  ya  fasihi  ya  Kiswahili  ni  mwandishi  wa vitabu  vya
          FOR ONLINE READING ONLY
              mashairi, tamthiliya,  hadithi/hadithi  za watoto, riwaya na kazi nyingine za
              kiubunifu kujipatia kipato. Vitabu hivi huingizwa kwenye soko la vitabu ambapo
              huweza kununuliwa na kusomwa na watu mbalimbali ndani na nje ya nchi, ambapo
              mwandishi hujipatia kipato na kujikimu maisha yake. Vilevile kupitia fursa hii,
              mwandishi anaweza kupata umaarufu kutokana na kazi yake na ambapo anaweza
              kupata fursa ya kualikwa kwenye makongamano mbalimbali ya kiubunifu, jambo
              ambalo huweza kumsaidia kumwongezea uzoefu. Kadhalika, kazi bora za fasihi
              huweza kuingia katika ushindani wa tuzo mbalimbali za kitaifa na kimataifa.
              Zinaposhinda,  mwandishi  hutunukiwa tuzo  ambazo aghalabu  huambatana  na
              kipato.


              Fursa nyingine ya mwandishi wa kazi za kifasihi ni kuuza nakala laini za kazi
              zake  katika  mitandao  ya kijamii,  hivyo kujipatia  kipato.  Mwandishi anaweza
              kuamua kufungua jukwaa la mtandaoni kwa ajili ya kurusha kazi mbalimbali
              za fasihi alizotunga. Pia, anaweza kuingia mikataba na wamiliki wa vituo vya
              runinga, redio na vyombo vingine vya habari na kupeleka kazi zake kwa ajili
              ya kusomwa, kutazamwa na kusikilizwa na jamii. Fursa zote hizi si kwamba
              humnufaisha mwandishi kwa kipato tu bali huweza kumpa umaarufu, hivyo watu
              kupenda kazi zake. Hali hii humhamasisha mwandishi kutunga kazi nyingi zaidi
              ambazo zitainua uchumi binafsi na wa kitaifa.

              Kazi za kifasihi zinaweza kuchapishwa katika magazeti mbalimbali ya ndani na
              nje ya nchi. Mwandishi anaweza kuingia mikataba na wamiliki wa makampuni
              ya magazeti kwa ajili ya kuchapisha hadithi, riwaya, mashairi na kazi nyingine za
              kifasihi kwa ajili ya kusomwa na jamii. Uzuri wa kazi husika unaweza kusababisha
              kuwa na wafuasi wengi wa kazi hizo, suala linalomuwezesha   mwandishi
              kujipatia kipato na umaarufu katika jamii. Kwa mfano, hadithi zilizoandikwa na
              Eric Shigongo zilipendwa na watu wa rika mbalimbali, kiasi cha kumwongezea
              kipato na kumpa umaarufu mkubwa.

              Uandishi wa kifasihi unaweza pia kumwezesha mtu kuwa mtaalamu wa kuhariri
              makala na vitabu vya fasihi ya Kiswahili. Uandishi huo hutoa fursa kwa mhariri
              kuwa na nafasi ya kusoma na kuhariri kazi binafsi au za mwandishi mwingine.
              Hii husaidia kuboresha ubunifu, ubora wa lugha, muundo, maudhui na mtiririko
              mzuri wa andiko husika kabla ya kuchapwa. Hii ni fursa nzuri katika kuimarisha


               146                                                 Kitabu cha Mwanafunzi
                                                                     Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   146                   23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   146
   152   153   154   155   156   157   158   159   160   161   162