Page 153 - Fasihi_Kisw_F5
P. 153

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari






                    Sura

                      ya                  Kubuni kazi changamani
               binafsi na cha jamii kwa ujumla.READING ONLY
                     Sita                               za fasihi






                          Utangulizi

               Kazi za fasihi ni muhimu katika jamii kwa sababu huburudisha, huelimisha,

               hueneza tamaduni mbalimbali na huchochea mawazo mapya kwa wasomaji.
               Katika  sura hii, utajifunza juu ya miktadha inayochagiza utunzi wa kazi
               changamani za fasihi, fursa zinazotokana na kazi za fasihi; na mchango wa
               TEHAMA katika kutambua fursa zinazotokana na kazi za fasihi. Pia, utajifunza
               hatua na kanuni za utunzi, na kutunga kazi za fasihi simulizi na fasihi andishi.
               Umahiri utakaojenga katika sura hii utakuwezesha kutunga maigizo, mashairi
          FOR ONLINE
               na hadithi za watoto; na kuzitumia kazi hizo kama fursa ya kujipatia kipato





                            Namna utunzi wa kazi za fasihi zinavyochochea maendeleo
                            binafsi na ya taifa kwa ujumla



               Shughuli ya 6.1

              (a)  Kwa kutumia  vyanzo  vya  mtandaoni  na  maktabani,  eleza  miktadha
                   inavyochagiza utunzi wa kazi za kifasihi.

              (b)  Kwa kutumia vyanzo vya mtandaoni au maktabani, kusanya kazi tano (5)

                   za fasihi za tanzu tofauti kisha chunguza na chambua miktadha iliyoziibua.

              Miktadha ya utunzi wa kazi changamani za fasihi
              Kazi za kifasihi ni matini ambazo hutumia lugha, ubunifu na vionjo vya kifasihi.
              Kwa hiyo, kazi hizo ni matini  ambazo  huwasilishwa kwa ubunifu. Kazi hizi
              hutofautiana na kazi nyingine zisizo za kifasihi kutokana na mbinu za uandishi
              kama vile uundaji wa wahusika na matumizi ya lugha ya kisanaa. Kazi za kifasihi



               142                                                 Kitabu cha Mwanafunzi
                                                                     Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   142
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   142                   23/06/2024   17:54
   148   149   150   151   152   153   154   155   156   157   158