Page 148 - Fasihi_Kisw_F5
P. 148

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




                                           ya Awali ya Sanaa katika Ualimu, nikizamia somo
                                           la Kiswahili.

                   Mwenyekiti wa Jopo:      Vyema. Kwa nini umeomba nafasi hii ya kazi?
          FOR ONLINE READING ONLY
                   Nagona:                   Nimeomba nafasi hii ya kazi ya kuwa msaidizi wa
                                           ukufunzi katika chuo hiki kwa sababu nina uwezo
                                           na ninapenda kutumia  elimu na taaluma  yangu
                                           kuwasaidia wengine kupitia taasisi hii.

                   Mwenyekiti wa Jopo:      Bi. Nagona, kuna taasisi nyingi ambazo ungeweza
                                           kuzitumia  kutimiza  shabaha  na  mapenzi  yako
                                           hayo, kwa nini iwe taasisi hii?

                   Nagona:                  Ndugu mwenyekiti,  nimependa  kuwa hapa kwa
                                           sababu mbili. Mosi, hii ni taasisi ya ndoto yangu
                                           kwa sababu siku nyingi nimekuwa nikiota kufanya
                                           kazi  hapa.  Pili,  ni sababu ya kuwapo kwa hiyo
                                           ndoto.  Nimekuwa  nikiifuatilia  taasisi  hii  tangu
                                           nikiwa katika hatua za chini za elimu; na nimekuwa
                                           nikishuhudia jinsi taasisi hii ilivyo tegemeo la taifa
                                           kwa kuzalisha  wataalamu  wa kada  mbalimbali.
                                           Hivyo, nikapata shauku ya mimi kuwa mmoja wa
                                           wapishi wa wataalamu hao. Sababu ya tatu ndugu
                                           Mwenyekiti ni kuwa taasisi hii imekuwa ya kwanza
                                           kutoa tangazo la kazi tangu nihitimu. Hivyo, kama
                                           wasemavyo wahenga kuwa, “mvua za kwanza ndo
                                           za kupandia”, nami niliona niichangamkie mvua
                                           hii ya kwanza kunyesha kwa muktadha wa kusaka
                                           ajira.


                   Mwenyekiti wa Jopo:      Karibuni wajumbe tumuulize maswali msailiwa.

                   Mjumbe 1:                Bi. Nagona, una kipi cha kutushawishi kuwa wewe
                                           ni bora kuliko waombaji wengine wa nafasi hii?

                   Nagona:                   Ndugu Mwenyekiti na jopo zima, ninawahakikishia
                                           kuwa mimi ni bora kuliko wengine kwa sababu
                                           zifuatazo:  Mosi, matokeo  yaliyomo  katika  vyeti
                                           vyangu vya elimu  na taaluma  yananibainisha



                     Kitabu cha Mwanafunzi                                           137
                        Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   137                   23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   137
   143   144   145   146   147   148   149   150   151   152   153