Page 147 - Fasihi_Kisw_F5
P. 147

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




              (b)  Kwa kutumia  misingi  ya ujenzi  wa hoja  zenye  mantiki  na ushawishi,
                   tathimini matendo ya wahusika katika tamthiliya teule mbili.

              Kuwasilisha hoja zenye mantiki na ushawishi kwa kutumia maarifa
              ya kifasihi
          FOR ONLINE READING ONLY
              Maarifa ya kifasihi hujumuisha umilisi wa vipera mbalimbali vya fasihi simulizi
              na andishi. Kazi yoyote ya fasihi huwa na mambo yanayoweza kutumiwa katika
              maisha halisi. Miongoni mwa matumizi hayo ni kujengea hoja zenye mantiki
              na ushawishi. Mjenzi wa hoja za kimantiki huweza kutumia vipera kama vile
              methali,  hadithi,  na  tamathali  za  semi  ili  kukazia  au  kunogesha  hoja  yake.
              Jambo muhimu ni mjengahoja kuteua kipengele cha kifasihi ambacho ni sahihi
              na muafaka katika muktadha wa hoja yake. Kwa ujumla, maneno, vifungu na
              tungo za kifasihi huwa na mvuto na mguso wa kipekee. Kutokana na mguso
              huo, zikitumiwa kwa usahihi sambamba na misingi ya kujenga hoja za kimantiki,
              hurahisisha kueleweka na kushawishi hadhira. Hoja zenye mantiki na ushawishi
              zinaweza  kutumiwa na watu katika  sehemu mbalimbali  wakati wa kueleza
              au kuomba kitu fulani. Sehemu ambazo hoja za kimantiki hutumika ni kama
              vile kwenye usaili wa kazi au kwenye malumbano ya hoja. Maelezo yafuatayo
              yanafafanua namna hoja za kimantiki na zenye ushawishi zinavyotumika katika
              usaili na malumbano ya hoja.


              Kutumia maarifa ya kifasihi kuwasilisha hoja zenye mantiki na ushawishi
              katika usaili

               Shughuli ya 5.12

              (a)  Soma dayalojia ifuatayo ya usaili, kisha jibu maswali yanayofuata:
                   Mwenyekiti wa Jopo:     Jitambulishe tafadhali.


                   Msailiwa:                Ninaitwa Nagona Dhifa Mzingile. Nina miaka 26.
                                           Nimezaliwa na kukulia wilayani Songea, mkoani
                                           Ruvuma. Nilianza masomo ya msingi mwaka 2005
                                           katika  Shule ya Msingi Mpangula  na kuhitimu
                                           mwaka 2011. Kisha, nikajiunga  na elimu  ya
                                           sekondari  katika  Shule ya Sekondari  Namtumbo
                                           na  kuhitimu  mwaka  2015.  Baada  ya  hapo,
                                           nilisoma elimu ya sekondari ya juu katika Shule
                                           ya Sekondari ya Wasichana Songea na kuhitimu
                                           mwaka 2018. Baadaye, nilijiunga na masomo ya
                                           juu, ambapo mwaka 2023 nilitunukiwa Shahada



               136                                                 Kitabu cha Mwanafunzi
                                                                     Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   136
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   136                   23/06/2024   17:54
   142   143   144   145   146   147   148   149   150   151   152