Page 142 - Fasihi_Kisw_F5
P. 142

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




                   (ii)  Ni mbinu zipi za kifasihi zimekutatiza kupata maana katika shairi hili?

                   (iii)  Una maoni gani kuhusu kufaa au kutofaa kwa mbinu za kifasihi
                        zilizotumika katika shairi hili ili kuleta maana?
                   (iv)  Mstari  unaosema  ‘Mbaya wetu  karudi,  shetani  rangi  rangile’ una
          FOR ONLINE READING ONLY
                        maana gani?


              (b)  Kwa kutumia  diwani  teule,  chambua  shairi  moja,  kisha  onesha  namna
                   mbinu za kifasihi zilivyochangia au kutatiza kupatikana kwa maana.
              Mbinu za kifasihi zinavyoathiri kupatikana kwa maana katika tamthiliya

               Shughuli ya 5.9
              Soma matini fupi ya tamthiliya ifuatayo, kisha chambua namna mbinu za kifasihi
              zinavyoathiri maana.

                   Moyo:   [Anaitazama hali iliyowazunguka]


                              Nani wa kulaumiwa? Kati ya mpunga uliosababisha viroboto au
                            mwenye mguu anayeshindwa kutoa funza?

                            [Anazama kwa tafakuri nzito].

                   Macho:   wote.


                   Moyo:   Ikiwa wote, tupe sababu kuntu. Kwa nini?

                   Macho:   Wote wanaonekana. Mimi ninalaumu kila anayeonekana.

                              Ndani joto ni kali sana, nasema na nje baridi ni kali sana sitakaa
                            kimya.

                   Akili:      Hahahah! [Kicheko], wanadunga wa kwetu, wao wanauza.


                              Masomo yao moshi ni sumu ya kwetu moshi ni chakula, twala na
                            hatushibi.

                   Moyo:    Nani alaumiwe?  Someni pale  “Ni hatari kwa mustakabali
                            wako.” Haya niambieni, nani alaumiwe? Anayetoa ujumbe ule
                            ndiye anayekusanya kodi kutoka palepale.


                             [Anaonesha kwa kidole].




                     Kitabu cha Mwanafunzi                                           131
                        Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   131                   23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   131
   137   138   139   140   141   142   143   144   145   146   147