Page 137 - Fasihi_Kisw_F5
P. 137

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




              hupendwa na kila mtu ndani ya familia.  Sauti yake ni ulinzi tosha dhidi ya
              wapangaji wanaochungulia na kudokoa mali ya binadamu.

              Rangi nzuri inayovutia pamoja na macho yake mithili ya gololi ni baadhi ya
              vitu vinavyompa upekee. Paka ni doli la watoto na kitulizo murua cha watoto
          FOR ONLINE READING ONLY
              dhidi ya adui zao. Kiumbe huyu hukunja kucha zake vizuri ili zisimdhuru mtoto
              aliyembeba.  Adabu hii amefundishwa na mama  yake, ndio maana  wahenga
              wanasema samaki mkunje angali mbichi.


              Paka wetu ni mwaminifu na mlinzi bora, kwake udokozi ni mwiko. Hana tabia ya
              kula chakula isipokuwa amewekewa kwenye chombo maalumu. Chakula chake
              ni maziwa, michuzi na mifupa ya samaki.


              Weledi  wa  kijasusi,  paka  amekirimiwa.  Huweza  kuwapigisha  kwata  maadui
              aliowateka. Hawa ni wale wenye mipango ya kumpora binadamu. Paka huwaona,
              kisha hutembea kwa kunyata taa! Taa! Taa! Taa! Kisha kuwarukia na kuwakamata.

              Paka awapo vitani, hapati ngeu kichogoni. Ni jasiri ajabu! Asikiapo mlio wa
              nyoka siii! iiii! iiii! Hujipanga haraka kwa ajili ya kumdaka nyoka mithili ya
              golikipa.  Siku  moja,  tulisikia  vurugu  kali  juu  ya  dari,  kumbe  alikuwa  nyoka
              aliyekuwa  akipambana na paka. Paka alifanikiwa  kumuua nyoka mkubwa na
              kushuka naye kutoka darini.


              Usalama wa mali zetu upo mikononi mwa paka. Paka ana mbinu kabambe za
              kumdhibiti  rafiki  yake  aitwaye  Panya. Wakati  mwingine  humwimbia  nyimbo
              kama:


                   “Njoo tule nyama, njoo ×2

                   Nyama hiyooo!

                   Kimbiaaa!

                   Njoo tufurahi.”


              Paka hutumia mbinu hizi kuwarubuni panya na hatimaye kuwakamata. Mali zetu
              ambazo ni nguo, vitabu, daftari na viatu vina usalama wa kutosha kutokana na
              kuwapo kwa paka.

              Paka hukwea miti kwa maringo mithili ya kinyonga afukuzaye mawindo. Hapa





               126                                                 Kitabu cha Mwanafunzi
                                                                     Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   126                   23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   126
   132   133   134   135   136   137   138   139   140   141   142