Page 132 - Fasihi_Kisw_F5
P. 132

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




              (c)  Chambua mbinu zilizotumika kujenga ujumi katika mashairi  mawili ya
                   diwani teule ulizozisoma.

              Mbinu zilizotumika kujenga ujumi katika majigambo
          FOR ONLINE READING ONLY
               Shughuli ya 5.3
              (a)  Tamba au soma jigambo lifuatalo, kisha jibu maswali yanayofuata.

                   Jabali
                   Mimi ni jabali

                   Naangamiza kama umeme unavyopasua anga

                   Wenye shari wote huniogopa

                   Mafedhuli na mahayawani hufichama wakiniona
                   Kila dhalimu hunigwaya na kunikimbia

                   Mimi ni kama jahazi linalopambana na mawimbi baharini

                   Gharika ikishavuma hurudi kuwa wima

                   Yote yenye mawaa hukimbia kutokomea

                   Wengi kushangaa jabali kuwayumbisha
                   Madhalimu wote udhalimu hukoma

                   Matendo mema hutenda kuisalimisha dunia

                   Mimi ni jabali

                   kamwe sitetereki kwa lolote.

                   Maswali

                   (i)  Ni kwa namna gani taswira zimetumika kujenga ujumi katika jigambo
                        hili?

                   (ii)  Mbinu ya taharuki imetumikaje kujenga ujumi katika jigambo hili?

                   (iii)  Ni vifungu vipi vya maneno katika jigambo hili vinaakisi mbinu ya
                        uteuzi na mpangilio wa maneno?

                   (iv)  Ni mbinu zipi nyingine zilizotumika kujenga ujumi katika jigambo
                        hili?



                     Kitabu cha Mwanafunzi                                           121
                        Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   121                   23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   121
   127   128   129   130   131   132   133   134   135   136   137