Page 130 - Fasihi_Kisw_F5
P. 130

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




                               Kila mtu lugha yake, ndiye mtumishi mwema,

                               Lugha nyingine makeke, mviringo kuzisema,
                               Kila mkuu na pake, hana hadhi akihama,
          FOR ONLINE READING ONLY
                               Kiswahili nivike, joho lako la heshima,

                               Titi la mama li tamu, jingine halishi hamu.




                               Lugha yangu ya utoto, hata leo nimekua,
                               Tangu ulimi mzito, sasa kusema najua,

                               Sawa na manukato, moyoni mwangu na pua,

                               Pori, bahari na mto, napita nikitumia,

                               Titi la mama li tamu, jingine halishi hamu.



                               Kiswahili kikikopa, lugha nyingine pia,

                               Ambazo zimenenepa, jambo hili hutumia,

                               Au sivyo zingetupwa, kwa kukosa manufaa,

                               Kiswahili kikikopa, si ila ndiyo tabia,
                               Titi la mama li tamu, jingine halishi hamu.



                                    Pambo la Lugha (Robert, 1973:27-29)

                   Maswali

                   (i)  Unafikiri kwa nini mwandishi amefananisha Kiswahili na titi la mama?

                   (ii)  Ni mbinu zipi za kiujumi zilizotumika katika shairi hili?

                   (iii)  Ni kipengele kipi cha ujumi wa kijadi kinachojitokeza katika shairi
                        hili?
                   (iv)  Katika ubeti wa pili, mwandishi anakusudia nini anapotaja lugha za
                        Kiarabu, Kirumi na Kiingereza?

                   (v)  Ni dhana zipi zinazodhihirisha uzuri na ubaya wa shairi hili?



                     Kitabu cha Mwanafunzi                                           119
                        Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   119                   23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   119
   125   126   127   128   129   130   131   132   133   134   135