Page 126 - Fasihi_Kisw_F5
P. 126

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




                   (v)  Ni kwa namna gani matendo ya wahusika Vera na Avita yanasawiri
                        matendo yanayofanywa na watu katika jamii?

                   (vi)   Kiimani na kimtazamo mhusika Beti anawakilisha kundi lipi la vijana
                        katika jamii?
          FOR ONLINE READING ONLY
                   (vii) Una mtazamo gani wa jumla kuhusu matini hii?


              (b)  Jadili athari za kiimani  na kimitazamo  zilizomo  katika tamthiliya  mbili
                   teule, zinavyojitokeza katika jamii.

                   Tamrini
                   1.   Jadili namna athari za mitazamo ya wahusika wawili katika tamthiliya
                       teule mbili ulizosoma zinavyojitokeza katika jamii.

                   2.   Jadili uhusiano uliopo baina ya mitazamo iliyomo katika nyimbo mbili
                       za bongo fleva na matendo ya jamii.

                   3.   Linganisha masuala ya mitazamo  ya kijamii  kama yanavyosawiriwa
                       katika tamthiliya mbili teule.

                   4.   Jadili kauli kwamba “Nyimbo za bongo fleva hazina maadili kwa jamii”.


                   5.   Chambua maadili na mitazamo inayojitokeza katika mashairi mawili ya
                       diwani teule.

                   6.   Tumia nyimbo mbili za bongo fleva kulinganisha mitazamo iliyomo
                       katika nyimbo hizo na imani za jamii.

                   7.   Huku ukilinganisha na imani za jamii, jadili maadili yanayopatikana
                       katika tamthiliya mbili teule.

                   8.   Maadili na imani za jamii zinachangia katika utunzi wa kazi za fasihi
                       hususani nyimbo na tamthiliya. Jadili kauli hii kwa kutumia mashairi
                       mawili (2) kutoka katika diwani teule.

                   9.   Sikiliza  nyimbo  mbili  za  bongo  fleva  uzipendazo,  kisha  chambua
                       maadili yaliyomo katika nyimbo hizo.

                   10.  Athari za kiimani na kimtazamo huweza kuimarisha au kudumaza kazi
                       za kifasihi. Jadili kauli hii kwa mifano kuntu.





                     Kitabu cha Mwanafunzi                                           115
                        Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   115                   23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   115
   121   122   123   124   125   126   127   128   129   130   131