Page 123 - Fasihi_Kisw_F5
P. 123

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




              Athari za kiimani na kimtazamo katika bongo fleva zinavyojidhihirisha
              katika jamii
              Kuna athari nyingi za kiimani na za kimtazamo zinazotokana na maudhui ya
              nyimbo  za  bongo  fleva.  Kwa  kuwa  utanzu  huu  hutumia  zaidi  redio,  runinga
          FOR ONLINE READING ONLY
              na mitandao ya kijamii, inakuwa rahisi kwa athari za imani na mitazamo hiyo
              kuifikia hadhira kwa haraka. Athari hizo huweza kujenga ama kubomoa jamii
              zisipopokelewa kwa tahadhari na uchambuzi faafu.

               Shughuli ya 4.15

              (a)  Kwa kutumia vyanzo vya mkondoni na vinginevyo, sikiliza  wimbo wa
                   msanii yeyote wa kike unaohamasisha mapambano ya maisha, kisha jibu

                   maswali yafuatayo:
                   (i)  Ni mitazamo na imani ipi inapatikana katika wimbo huo?

                   (ii)  Wimbo huo unatoa taswira gani kuhusiana na changamoto za kiuchumi
                        na maisha ya kila siku katika jamii?
                   (iii)  Wimbo huo una athari zipi za kiimani na kimtazamo katika jamii?

                   (iv)  Wimbo huo una athari zipi za kiimani na kimtazamo kwa vijana?

                   (v)  Ni mitazamo ipi iliyomo katika wimbo huo haiendani na jamii? Kwa
                        nini?
                   (vi)  Ni mafunzo gani jamii inaweza kuyapata kutokana na wimbo huo?

                   (vii) Una mtazamo gani kuhusu wimbo huo ukilinganisha na maisha ya kila
                        siku?

              (b)  Jadili namna athari za kiimani na mitazamo katika nyimbo mbili za bongo

                   fleva (kongwe na za sasa) zinavyojitokeza katika jamii.

              Athari  za  kiimani  na kimtazamo  katika mashairi  zinavyojitokeza  katika
              jamii
              Fasihi  andishi,  ukiwamo  utanzu  wa ushairi,  husawiri  imani  na  mitazamo  ya
              jamii  katika  kutoa  maudhui.  Maudhui  hayo  huchagiza  ufanisi  na  mabadiliko
              yanayohitajika. Kwa njia hii, mashairi huibua mitazamo na imani ambazo huweza
              kuchangia ustawi wa jamii husika.








               112                                                 Kitabu cha Mwanafunzi
                                                                     Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   112
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   112                   23/06/2024   17:54
   118   119   120   121   122   123   124   125   126   127   128