Page 122 - Fasihi_Kisw_F5
P. 122

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




                   Che Munndu:        Wasomeshe basi hao watoto wako. Nani anataka hasara?
                                    Unapeleka watoto shule siku mbili wamepata mimba.

                   Bi Somoe:         Lakini si nyie wenyewe ndo mwawapa mimba?  We
                                    mwenyewe mbona mwaka juzi ulioa binti ndogo wa shule.
          FOR ONLINE READING ONLY
                                    Lakini sharia zipo, iko siku zitachukua nkondo wake.

                   Che Munndu:        Sheria  sheria  ndo  kitu  gani?  Wangapi  hapa  kijijini
                                    wamewapa watoto wa shule mimba. Na hatuoni kufungwa?
                                    Si mnawafundisha watoto wenu wenyewe (huku akibana
                                    pua) ‘bwana  aliyenipa  mimba  sinjui’.  Sasa  hiyo  akili
                                    kweli? Hela yangu si afadhali nkaoe nke mwingine.
                                    Kuliko kupeleka ntoto shule anayeishia kupata mimba na
                                    kuniongezea nzigo?


                                           Safari ya Chinga (Omari, 2012: 18 – 20)

                   Maswali

                   (i)  Mwandishi anabainisha  mitazamo  gani katika  kipande hiki cha
                        tamthiliya?
                   (ii)  Una maoni gani kuhusu mitazamo iliyomo katika kipande hiki cha
                        tamthiliya? (Toa sababu)

                   (iii)  Unafikiri mtazamo wa mhusika Bi. Somoe una uhalisi katika jamii?
                        Kwa nini?

                   (iv)  Je, unadhani mtazamo  wa Che Mundu wa kujitenga na jukumu la
                        kumuelimisha mtoto unasawiri matendo ya jamii yako?
                   (v)  Ni kwa namna gani mitazamo  ya mhusika Che Mundu inaathiri
                        matendo ya jamii?

                   (vi)  Je, jamii yako ina mitazamo gani kuhusu mimba za utotoni?

                   (vii) Unafikiri kuna uhusiano wowote kati ya mitazamo ya wahusika wa
                        tamthiliya hii na matendo ya jamii? Toa sababu.

              (b)  Kwa kutumia tamthiliya  mbili  teule ulizosoma, husianisha mitazamo
                   iliyomo katika tamthiliya hizo na matendo ya jamii.







                     Kitabu cha Mwanafunzi                                           111
                        Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   111                   23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   111
   117   118   119   120   121   122   123   124   125   126   127