Page 127 - Fasihi_Kisw_F5
P. 127

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari






                    Sura

                      ya                Ujumi katika kazi za fasihi
          FOR ONLINE READING ONLY
                    Tano






                          Utangulizi

               Ujumi ni dhana inayotumika duniani kote japo wananadharia na wanajamii

               hutofautiana kimtazamo kuhusu dhana hii. Mijadala kuhusu ujumi hujitokeza
               katika nyanja tofauti, miongoni mwa nyanja hizo ni fasihi andishi na simulizi.
               Katika sura hii, utajifunza kueleza na kuchambua mbinu za kiujumi katika
               kazi za fasihi za majigambo, mashairi na tamthiliya teule. Aidha, utajifunza
               jinsi mbinu za kifasihi zinavyoathiri kupatikana kwa maana katika kazi hizo.
               Kadhalika,  utajifunza  namna  ya  kutumia  fasihi  katika  kujenga  hoja  zenye
               mantiki na ushawishi. Umahiri utaoujenga utakuwezesha kutambua na kueleza

               ujumi katika miktadha mbalimbali.




                            Namna uchambuzi wa ujumi unavyoboresha utunzi wa kazi
                            za fasihi




               Shughuli ya 5.1
              Kusanya nyimbo tano (5) za bongo fleva ambazo, kwa maoni yako, ni nzuri na
              nyimbo tano (5) ambazo, kwa maoni yako, ni mbaya; kisha, kwa kila wimbo
              eleza kwa nini unaona ni mzuri au mbaya.


              Ujenzi wa ujumi katika kazi za fasihi
              Dhana ya ujumi imejadiliwa na wataalamu mbalimbali kwa mfano Zirimu na
              Gurr (1971), Nyirenda na Ishumi (2002), Ponera (2014), na Habwe na Zaja (2019)
              ambao wanaeleza kuwa ujumi ni hisia za akilini au ni misingi ya kifalsafa kuhusu
              uzuri wa sanaa. Wanaongeza kuwa ujumi sharti uendane na jamii mahsusi kwa
              lengo mahsusi la kazi ya kisanaa inayobuniwa. Nyirenda na Ishumi (2002) wote



               116                                                 Kitabu cha Mwanafunzi
                                                                     Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   116
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   116                   23/06/2024   17:54
   122   123   124   125   126   127   128   129   130   131   132