Page 131 - Fasihi_Kisw_F5
P. 131

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




              (b)  Chambua mbinu zilizotumika kujenga ujumi katika shairi lifuatalo.

                         Ukurasa wa Mwisho
                         Nimesoma visa vya mazonge ya vituko, mazinge ya njia;
          FOR ONLINE READING ONLY
                         Visa vya ndoto zenye matundu, macho mia yanayougua;

                         Visa vya pesa kuzidi kujaa kwenye mifuko is’ojaa;
                         Na ukata kustakimu ubavuni pa ukwasi dawamu;

                         Nimevisoma na kusaili;

                            Ukurasa wa mwisho haupo?
                         Nimesoma visa vya wakata misitu ya majoka yatishayo;

                         Visa vya mazimwi yalayo watu, na vifisi na vibweha vyayo;

                         Visa vya kina Masalakulangwa - adui wa mazimwi hayo;
                         Visa vya wajenzi nyumba mpya, na walimaji mashamba mapya;

                         Nimevisoma na kung’amua:

                            Ukurasa wa mwisho haupo.
                         Nimesoma ngano isiyokuwa na mwisho - ya maendeleo

                         Ya mnyonge katika mazonge ya mawimbi ya bahari leo;

                         Ngano ngumu ya sanaa ya harakati iwashayo mifuo
                         Ya jasho na nyundo na risasi, - tabaka kuasi kwa visasi

                         Nimesoma, na sasa nakiri:

                            Ukurasa wa mwisho haupo.
                         Nimezisoma pia ngano za kale zisizosahaulika

                         Za matamanio yasiyokauka, na ari is’ovunjika;

                         Nimesoma jinsi ya kufumbua ishara zilizofumbika;
                          Nazidi kufunua kurasa, nazidi kufasiri mikasa:

                         Nimesoma, na sasa nasema:

                            Ukurasa wa mwisho haupo.

                       Kunga za Ushairi na Diwani Yetu (Kahigi na Mulokozi, 1979:118-119)



               120                                                 Kitabu cha Mwanafunzi
                                                                     Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   120                   23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   120
   126   127   128   129   130   131   132   133   134   135   136