Page 135 - Fasihi_Kisw_F5
P. 135

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




                   (iv)  Ni vifungu vipi vya maneno katika tamthiliya hii vinaakisi mbinu ya
                        uteuzi na mpangilio wa maneno?

                   (v)  Ni mbinu zipi nyingine za kiujumi zimetumika katika matini hii?
          FOR ONLINE READING ONLY
              (b)  Chambua mbinu zilizotumika kujenga ujumi katika tamthiliya teule mbili
                   ulizosoma.

              Maana na matumizi ya lugha katika matini za fasihi
              Kazi yoyote ya fasihi huwa na maana. Mtunzi hukusudia kuwasilisha ujumbe
              fulani kwa hadhira anayoilenga. Matini ya kifasihi hutofautiana na matini isiyo
              ya kifasihi (kama vile taarifa ya habari iwasilishwayo katika chombo cha habari)
              kutokana na matumizi ya lugha ya kifasihi. Lugha hiyo ya kifasihi hupatikana
              kutokana na matumizi ya mbinu za kifasihi. Baadhi ya mbinu hizo ni: semi (kama
              vile methali na nahau), tamathali za semi (kama vile sitiari, majazi, tashibiha, na
              tashihisi), mafumbo, lugha ya ishara na alama, na uteuzi na mpangilio maalumu
              wa maneno. Kutokana na matumizi ya mbinu hizi, matini ya kifasihi huwa na sifa
              ya kufikirisha kuliko matini isiyo ya kifasihi. Pia, mbinu hizo huifanya kazi ya
              fasihi iwe na mvuto kwa hadhira yake.

              Hali ya hadhira kuwa na uwezo tofauti pamoja na kuwapo kwa lugha ya kifasihi
              katika matini husababisha hadhira kuibua maana  tofauti katika  matini  moja.
              Hivyo, ili hadhira ipate maana iliyokusudiwa, hutakiwa kuwa na uwezo wa
              kung’amua maana mbalimbali ambazo zimefumbatwa katika mbinu hizo. Maana
              huweza kujitokeza katika kazi za kifasihi kama vile insha za kifasihi, mashairi na
              tamthiliya kama ifuatavyo:

              Maana zinazopatikana katika insha za kifasihi

               Shughuli ya 5.5
              (a)  Soma insha ifuatayo, kisha jibu maswali yanayofuata.

                   Uongo
                   Uongo ni kinyume cha hakika ya mambo yaliyokuwa au yalivyo. Ni
                   watu wachache ambao si waongo katika dunia.  Watakaokudanganya  au
                   kukupunja hutumia uongo. Huweza kumsaidia mtu kujiokoa pengine, lakini
                   ni mamoja yote kuwa uongo ni tabia mbaya na si kitu cha kupendelea katika
                   maisha. Uongo hautazamiwi kwa watu waovu na wajinga peke yao, hata
                   watu wema na wataalamu huutumia. Bahari moja ya hatari katika dunia ni
                   uongo. Mwongo mmoja huweza kuangamiza watu kadha wa kadha. Uongo
                   wa wajinga hugunduliwa upesi sana kuliko ule wa wataalamu. Baadhi ya


               124                                                 Kitabu cha Mwanafunzi
                                                                     Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   124
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   124                   23/06/2024   17:54
   130   131   132   133   134   135   136   137   138   139   140