Page 138 - Fasihi_Kisw_F5
P. 138

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




              hunoa mikuki yake tayari kwa mawindo na maadui. Wakati wa burudani hufanya
              mazoezi ya kupanda juu ya miti mirefu.

              Ninawashauri  watu  wasiwapige  paka  kwa mawe;  badala  yake,  wawajali  na
              kuwapatia mahitaji yao kama vile: chakula, maziwa, nyama na maji. Paka ni
          FOR ONLINE READING ONLY
              mfalme kwa watu wenye busara ya kujali viumbe. Urafiki wa binadamu na paka
              unapaswa kuwa wa kudumu. Wanyama wengine hawana budi kuiga matendo ya
              paka ili kudumisha urafiki na binadamu.

               Shughuli ya 5.6

              (a)  Soma shairi lifuatalo, kisha jibu maswali yanayofuata.

                    Kifo cha Mende Wekundu

                    Na ujenge yako nyumba, jingi jasho likuoshe,

                    Ufyeke, upime na uweke nguzo,
                    Kisha paa na uweke na ukandike,

                    Siku nyingi bila kuingiliwa na mgeni hutakaa.

                    Wataanza kutalii mipaka mende usiku,

                    Nje na ndani ya nyumba watazunguka,

                    Bila woga, bila ruhusa ulichonacho watakula,
                    Masalia yatakuwa yako, ijara ya kaziyo.

                    Na nyingi dawa uweke, nyumba nzima uihame,

                    Ukae nje nzima siku usubiri,

                    Wazima wamelala ukirudi usiku,

                    Vichwa ngumu hawafi mende rahisi.
                    Kifo cha mende sharti miguu juu,

                    Kichwa ukikanyage kipasuke usikie,

                    Na kisha wengine usiku mchana uwasake,

                    Mpaka watakapokwisha. Usiseme nao.

                            Karibu Ndani (Kezilahabi, 1988:33)




                     Kitabu cha Mwanafunzi                                           127
                        Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   127                   23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   127
   133   134   135   136   137   138   139   140   141   142   143