Page 141 - Fasihi_Kisw_F5
P. 141

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




              Mbinu za kifasihi zinavyoathiri kupatikana kwa maana katika kazi za
              fasihi
              Katika machakato wa usomaji, huweza kuibuka maana tofauti kwa kila msomaji.
              Jambo, hili huweza kutokana na jinsi msomaji anavyofasili taswira mbalimbali
          FOR ONLINE READING ONLY
              zilizotumiwa. Kuwapo kwa uwezekano wa kupatikana kwa maana mbalimbali
              kunatokana na mtunzi kutumia mbinu ya kifasihi ya ufumbaji. Hii inamaanisha
              kuwa, kama mtunzi asingefumba, maana ingekuwa ya wazi na ya moja kwa moja.
              Hivyo, kuwapo kwa maana tofauti kunatokana na mbinu za uandishi na utungaji
              ambao hufasiliwa kwa njia tofauti kwenye sehemu au kazi nzima ya kifasihi.
              Mbinu za kifasihi hutumika katika kazi mbalimbali za kifasihi kulingana na nini
              mtunzi anapenda kuandikia. Mbinu hizo zinabainika katika shughuli ifuatayo.

              Mbinu za kifasihi zinavyoathiri kupatikana kwa maana katika mashairi

                Shughuli ya 5.8

              (a)  Soma shairi lifuatalo, kisha jibu maswali yanayofuata:

                             Shetani, Rangi Rangile
                             Aa, awali sisi twanena, sisi sisi wananchi,

                             Ama kiza twakiona, ni kiza hiki hakuchi,

                             Mbaya wetu karudi, karudi tena mbichi,

                             Huu ukweli nanena, kweli siyo pirikichi,
                             Mbaya wetu karudi, shetani rangi rangile.

                             Ba, bahari tunaiona, bado haina shuwari,

                             Mawimbi yatatizana, mkondoni menawiri,

                             Tufani ni nana nana, katu hatuoni heri,

                             Roho atuminya sana, ka jeuri na kiburi,
                             Mbaya wetu karudi, shetani rangi rangile.



                            Diwani ya Tunzo ya  Ushairi ya Ebrahim Hussein (Rashid, 2016:166)


                   Maswali
                   (i)  Ni mbinu zipi za kifasihi zimetumika kupata maana katika shairi hili?




               130                                                 Kitabu cha Mwanafunzi
                                                                     Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   130
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   130                   23/06/2024   17:54
   136   137   138   139   140   141   142   143   144   145   146